Saturday, January 19, 2013

Liverpool kumsaini Mbrazil, Zaha Jumatatu ni Man au Arsenal, Big Sam kwa Pilato!!


SAM_ALLARDYCE 




















Klabu ya Liverpool iko mbioni kumsaini Chipukizi wa Barazil Philippe Coutinho huku hatima ya Kinda wa Crystal Palace, Wilfried Zaha, kujulikana Jumatatu na Meneja wa West Ham, Sam Allardyce, amefunguliwa mashitaka na FA, Chama cha Soka England, kwa kukiuka Kanuni kufuatia kauli yake dhidi ya Refa aliechezesha Mechi yao na Manchester United.
Liverpool na Mbrazil
Liverpool wako mbioni kusaini Mchezaji wao wa Pili katika Dirisha hili la Uhamisho la Mwezi Januari baada ya kutoa Ofa ya Pauni Milioni 8 kumchukua Kiungo wa Inter Milan Philippe Coutinho.
Coutinho, Miaka 20, ambae ameichezea Brazil mara moja na alichukuliwa na Inter Milan akiwa na Miaka 16 tu na kubaki kwao Brazil kwa Mkopo hadi 2010 ambako ndio alitua Inter Milan na kucheza Mechi 28 lakini Msimu uliopita alipelekwa Spain kuchezea Espanyol kwa Mkopo.
Mchezaji mwingine alienunuliwa na Liverpool hii Januari ni Straika kutoka Chelsea Daniel Sturridge aliechukuliwa kwa Dau la Pauni Milioni 12.
Zaha
Crystal Palace > Arsenal au Man United
Habari za ndani zimedokeza kuwa Uhamisho wa Wilfried Zaha wa Crystal Palace kwenda Manchester United au Arsenal utajulikana mwanzoni mwa Wiki ijayo.
Ingawa Man United ndio inayopewa nafasi kubwa kumchukua Kinda huyo, hasa baada ya Mtendaji Mkuu wa Klabu hiyo, David Gill, kukiri kuwa wamekuwa wakimfuatilia, lakini pia Arsenal wamekuwa wakimwinda.
Hata akiuzwa kwa sasa, Crystal Palace imekuwa ikisisitiza kipengele cha kubaki na Mchezaji huyo hadi mwishoni mwa Msimu ili awasaidie kuwapandisha Daraja.
Frazier
Sunderland > Cardiff City
Fraizer Campbell yupo mbioni kukamilisha Uhamisho wa £600,000 kutoka Sunderland kwenda Cardiff City.
Straika huyo wa zamani wa Manchester United ambae ameichezea England mara moja amekuwa akiandamwa na tatizo la Goti baada ya kuumia vibaya mara mbili katika Goti hilo hilo moja ambalo limemfanya kiwango kushuka.
Meneja wa Sunderland, Martin O'Neill, anategemewa kumnunua Danny Graham kutoka Swansea kwa Pauni Milioni 5 ili kumbadili Frazier Campbell.
M'Vila 
Rennes > QPR
Kiungo huyo wa Klabu ya Rennes ya France ambae anathaminiwa kwa Pauni Milioni 7 anawindwa na Meneja wa QPR Harry Redknapp lakini pia zipo Klabu nyingine zinazomwandama.
Akiongea kuhusu Yann M'Vila, Loïc Rémy amesema: "Ningependa aje QPR tuwe pamoja. Nishamwambia hapa ni pazuri."
Sam Allardyce ashitakiwa na FA
Meneja wa West Ham Sam Allardyce amefunguliwa Mashitaka ya Utovu wa Nidhamu na FA, Chama cha Soka England, kufuatia kauli yake mara baada ya Timu yake Jumatano iliyopita kufungwa Bao 1-0 na Manchester United na kutupwa nje ya FA CUP.
Alardyce alidai uamuzi wa kuwanyima Penati Uwanjani Old Trafford na kuwapa Man United Penati ni sababu ya kucheza Uwanja wa Nyumbani.
Hata hivyo Penati waliyopewa Man United ilipaishwa na Straika Wayne Rooney. Allardyce amepewa hadi Januari 23 kujibu Mashitaka hayo.
Penati ambayo West Ham wanaidai ni pale Fulbeki Rafael alipokontroli mpira na Paja na kisha kumgonga Mkononi.
Allardyce alikaririwa akisema: “Unaona kila mara Old Trafford! Hamna tofauti kati ya kushika kwa Rafael na Jordan Spence. Ila Spence anachezea West Ham, Timu ya ugenini na Rafael ni Mchezaji wa nyumbani Old Trafford.”
Taarifa ya FA imesema: “Shitaka hili linahusiana na kuvunjwa kwa Kanuni ya FA E3.”
CHANZO SOKA IN BONGO

No comments:

Post a Comment