MVUA
nyepesi iliyonyesha kuanzia alfajiri, jana haikuwazui mamia ya wafausi
wa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, kujitokeza kwa wingi katika
Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha, wakati mbunge huyo alipofikishwa
kusomewa shtaka la uchochezi.
Lema ambaye alikamatwa Ijumaa
usiku kwa amri ya Mkuu wa Mkoa, Magesa Mulongo, na kuwekwa rumande kwa
siku tatu, alifikishwa mahakamani saa tatu asubuhi akiwa katika gari dogo lenye vioo vyeusi likiwa na namba za usajili T 818 AJD.
Mbunge huyo alisindikizwa na askari wawili waliovaa suti wakiwa na silaha pamoja na Mkuu wa Upelelezi Mkoa (RCO).
Ilipofika saa nne, mbele ya Hakimu Devota Msofe, Mwendesha Mashtaka wa
Serikali, Elianenyi Njiro, alidai kuwa kesi hiyo ni mpya na inatajwa
mara ya kwanza, angeomba asome mashtaka na ipangiwe tarehe nyingine.
Akisoma mashtaka hayo, alidai kuwa Aprili 24, mwaka huu, katika eneo
la Freedom Square Chuo cha Uhasibu, Lema alichochea utendaji makosa na
kukiuka kifungu 390 na 35 cha kanuni za dhabu sura ya 16 kama
ilivyorekebishwa mwaka 2000.
Alitaja shtaka la Lema ni kutamka
maneno: “Mkuu wa mkoa anakwenda kwenye ‘send off’, hajui chuo cha
uhasibu mahali kilipo wala mauaji ya mwanafunzi wa chuo hiki. Ameshindwa
kuwapa pole kwa kufiwa na kusikiliza shida zenu na anasema hawezi
kuongea na wanafunzi wasio na nidhamu.” Alisisitiza kuwa maneno haya
ndiyo yaliyosababisha kuvurugika kwa amani.
Baada ya kusoma
shtaka hilo, aliongeza kuwa kwa upande wao hawana kipingamizi cha
dhamana na hivyo hakimu Msofe alimuuliza wakili wa mshtakiwa, Method
Kimomogolo, kama ana la kusema.
Kimomogolo alimueleza hakimu
kuwa kwa vile maelezo ya shtaka hayaonyeshi kuelekea kwenye kutenda
kosa, anaomba mshtakiwa aruhusiwe kujidhamini mwenyewe kwa kuwa ni
mbunge wa Arusha, hivyo hawezitoroka.
Hakimu Devota alitaja
masharti ya dhamana kuwa ni mdhamini mmoja mwenye kitambulisho na
atakaesaini dhamana ya sh milioni moja ambapo Diwani wa Viti Maalumu
(CHADEMA), Sabina Francis, aliitwa na Kimomogolo akamdhamini Lema baada
ya kukidhi masharti hayo.
Mara baada ya kukamilika kwa
taratibu hizo, hakimu Msofe aliahirisha kesi hiyo hadi Mei 29
itakapofika kwa ajili ya kutajwa tena.
Hali mahakamani
Lango la kuingilia katika chumba cha mahakama hiyo lilikuwa na askari
sita ambapo watatu walivalia mavazi rasmi wakiwa na silaha na wengine
wakiwa wanaangalia kila mtu anaekaribia hapo.
Askari wengine
waliovalia kiraia walikuwa ndani ya chumba cha mahakama wakiratibu kila
mtu aliyekuwemo ndani ambapo wengi waliokuwamo ni madiwani wa CHADEMA na
waandishi wa habari.
Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nasari, alikaa na Lema wakibadilishana mawazo juu ya kilichotokea.
Nje ya mahakama ambako wananchi wengi walikuwa wamekusanyika, nako kulikuwa na askari wengi waliokuwa wamevalia kiraia.
Mbali na askari kanzu kujaa mahakamani hapo pia askari waliovalia sare
wakiwa na gari tano huku wakisheheni silaha nzito pamoja na mabomu ya
machozi walifanya doria mahakamani na maeneo ya barabara zote za
kuelekea na kutoka eneo hilo.
Kulikuwa na magari yenye namba
za usajili PT 2077, PT 1076, PT 2017 na PT 1844, zote zikiwa na askari
wenye silaha kati ya saba na tisa wakizunguka maeneo yote jirani na
Mahakama Kuu mjini Arusha wakati katika Kituo Kikuu cha Polisi
kuliimarishwa ulinzi ambapo hakuna gari lililokuwa likiruhusiwa kuingia.
e
Lema ahutubia
Baada ya kesi kuahirishwa, wafuasi wa Lema waliandamana naye kutoka
katika viwanja vya mahakama na kupitia ofisi ya mkuu wa mkoa
wakishangilia hadi ofisi za CHADEMA mkoa.
Kutokana na wingi wa wafuasi hao ililazimu Lema kuzungumza nao katika kiwanja cha Shule ya Msingi Ngarenaro.
Aliwashukuru kwa kujitokeza kumuunga mkono na kuwasihi kuwa kamwe
wasiwe waoga katika kutetea haki zao mpaka wahakikishe nchi
inakombolewa.
Pia Lema alivishukuru vyombo vya habari kwa kuripoti ukweli halisi wa tukio na kusaidia kuepuka kubambikiwa mashtaka.
Alisema licha ya kuwekwa rumande lakini imemsaidia kujua masahibu
mengi wanayoyapata mahabusu wanapokuwa sero, kwamba kuna mahabusu wana
siku 26 hadi 40 hawajafikishwa mahakamani.
Alisema
ameshangazwa kukuta chumba cha kukaa watu 20 wanalazwa watu 90 kitendo
ambacho alidai kinahatarisha usalama wa mahabusu.
Lema alisema
kuwa hatokwenda bungeni wiki yote ili apate muda wa kufanya mikutano ya
hadhara huku akiwasisitizia wananchi wa Arusha mjini kumzomea mkuu wa
mkoa popote atakapokwenda.
“Nasisitiza ilikuwa ni haki yake
kuzomewa na wanafunzi wa Chuo cha Uhasibu kutokana na dharau
alizozionyesha alipofika chuoni hapo na nawaambia wakazi wa Arusha
kuendelea kumzomea popote atakapokwenda jimboni kwangu,’’ alisema.
Nao baadhi ya wananchi waliozungumza na MJUKUU WA TOZO baada ya Lema
kuachiwa walimlalamikia mkuu wa mkoa wakisema ametumia madaraka vibaya
pamoja na kumpotezea muda Lema wakati shtaka lenyewe halina mashiko.
Walisema kuwa ifike wakati uwekwe utaratibu wa kuwadhibiti viongozi
kama hao wanaochezea kodi za wananchi kwa mambo yasiyo na msingi.
Naye Nasari alimuonya Mulongo kuacha tabia ya kuwadharau wabunge wa
CHADEMA na kusema hali hiyo itamfanya ashindwe kuongoza mkoa huu.
Katibu wa CHADEMA Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa, mbali na suala
hilo la Lema alitoa tamko la chama kuitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi
kupitia kwa Mkurugenzi wa Jiji kuiunganisha kata ya Sombetini katika
uchaguzi mdogo utakaofanyika Juni 16.
Tuesday, April 30, 2013
Monday, April 29, 2013
LEMA AACHIWA KWA DHAMANA
wafuasi wa chadema wakiwa wanasubiria hukumu ya Mbunge wao nje ya mahakama kuu ya Arusha |
Mbunge wa Arusha
Mjini Godbless Lema ameachiwa kwa dhamana ya sh. milioni moja baada ya kushtakiwa kwa makosa ya uchochezi
katika mahakama ya Mkoa wa Arusha huku maandamano yakifanyika katika mitaa ya Jiji la Arusha.
Kesi ya uchochezi dhidi ya Lema imefunguliwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Mkoa wa Arusha na inaendeshwa na Hakimu Devota Msoffe
Kesi ya uchochezi dhidi ya Lema imefunguliwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Mkoa wa Arusha na inaendeshwa na Hakimu Devota Msoffe
Kesi hiyo imeahirishwa mpaka Mei 29 mwaka huu huku Katika
hati ya mashtaka ambayo ipo katika mahakama hiyo inasema kwamba kosa la Lema
ni kutoa maneno yanayodaiwa kuwa ni
uchochezi.
Baada ya hukumu hiyo mashabiki,
wafurukutwa na wanachama wa Chadema wamefanya maandamano makubwa kuelekea
katika ofisi za chama hicho ambazo zipo katika eneo la Ngarenaro mkoani humo.
Saturday, April 27, 2013
Mambo yaliyomfanya Mbunge wa arusha Godbless Lema akamatwe na kunyimwa dhamana jana
Mambo yaliyomfanya Mbunge wa arusha
Godbless Lema akamatwe na kunyimwa dhamana jana ni haya yafuatayo
baada ya kuongea na Mwanasheria wa Lema wakili Humphrey Mtui
i)Kosa la kwanza ni kuwaambia wanafunzi wa chuo cha uhasibu alipoenda kuwatuliza kuwa ‘dhambi kubwa kuliko zote ni woga ‘.Haki hutafutwa na kupiganiwa ikiwa jambo unalipigania ni la msingi na linafaa kupiganiwa(Worth fighting for)
ii)Kosa la pili ni pale alipotamka kuwa ‘’Tumemtafuta mkuu wa mkoa juu ya Matatizo yenu na mlivyoshuhudia hapa amechukua muda mrefu na kuingia kama vile anaingia kwenye send-off.Hawa ndiyo viongozi wetu ambao hawajali matatizo ya wananchi’’Kwa hiyo huo ni uchochezi
iii)Kosa la Tatu ni pale alipotamka kuwaambia wanafunzi kuwa ‘’Mimi Mbunge wenu nipo sambamba nanyi hadi mpate haki yenu na ikiwa mkuu wa mkoa hatakuja hapa kama mwenyekiti wa kamati ya ulinzi wa mkoa nitawaongoza hadi ofisini kwake ili mpate majibu na haki yenu kwani ni haki yenu ya msingi kwa mujibu wa katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ambayo niliapa kuilinda Bungeni na pia inaruhusiwa kwa mujibu wa kikanuni na kifalsafa katika utekelezaji wa utawala bora wa kidemokrasia ambao msingi wake ni kusikilizwa na kulinda haki za binadamu’’Huu nao umeitwa kwamba ni uchochezi.
i)Kosa la kwanza ni kuwaambia wanafunzi wa chuo cha uhasibu alipoenda kuwatuliza kuwa ‘dhambi kubwa kuliko zote ni woga ‘.Haki hutafutwa na kupiganiwa ikiwa jambo unalipigania ni la msingi na linafaa kupiganiwa(Worth fighting for)
ii)Kosa la pili ni pale alipotamka kuwa ‘’Tumemtafuta mkuu wa mkoa juu ya Matatizo yenu na mlivyoshuhudia hapa amechukua muda mrefu na kuingia kama vile anaingia kwenye send-off.Hawa ndiyo viongozi wetu ambao hawajali matatizo ya wananchi’’Kwa hiyo huo ni uchochezi
iii)Kosa la Tatu ni pale alipotamka kuwaambia wanafunzi kuwa ‘’Mimi Mbunge wenu nipo sambamba nanyi hadi mpate haki yenu na ikiwa mkuu wa mkoa hatakuja hapa kama mwenyekiti wa kamati ya ulinzi wa mkoa nitawaongoza hadi ofisini kwake ili mpate majibu na haki yenu kwani ni haki yenu ya msingi kwa mujibu wa katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ambayo niliapa kuilinda Bungeni na pia inaruhusiwa kwa mujibu wa kikanuni na kifalsafa katika utekelezaji wa utawala bora wa kidemokrasia ambao msingi wake ni kusikilizwa na kulinda haki za binadamu’’Huu nao umeitwa kwamba ni uchochezi.
Friday, April 26, 2013
FAHAMU KUHUSU KUKAMATWA KWA GODBLESS LEMA..SASA KUFIKISHWA KIZIMBANI JUMATATU
MAMBO yamezidi kumwendea kombo Mbunge wa Arusha Mjini, (Chadema) Godbless Lema baada ya Jeshi la Polisi kutangaza rasmi kwamba itamfikisha Mahakamani, siku ya Juma tatu.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa ArushaLiberatus
Sabas amema kwamba Mbunge huyo hawezi kuachilia huru kwa sababu
mashtaka dhidi yake yameshakamilika na atafikishwa Mahakamani siku ya
Juma tatau.
"Hatuwezi kumwachia kwa sababu anatarajia kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili"alisema Sabas.
Wakati
Kamanda huyo akitoa msimamo huo, taarifa za ndani ya Jeshi hilo
zinaeleza kwamba Mbunge huyo amehojiwa kwa zaidi ya saa nane sasa na
bado yuko katika chumba maalum kwa mahojiano zaidi na maofsa wa Polisi
huku akitakiwa kuonyesha ujumbe mfupi wa vitisho aliyodaiwa kuwa
ametumiwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Magesa Mulongo.
Katika
hatua nyingine Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Mkoa wa Arusha, kimekuwa
na kikao kirefu kinachoongozwa na Mkuu wa Mkoa Mulongo na kwamba ajenda
kubwa inayojadiliwa ni tukio zima la vurugu zilizotokea katika Chuo cha
Uhasibu mkoani humo. Lema
alikamatwa usiku wa kuamkia leo baada ya Askari wa Jeshi la Polisi
kumfuata nyumbani kwake na kuzingira nyumba yake kabla ya zoezi la
kumchomoa ndani ya nyumba hiyo kufanyika.
Mbunge
huyo anatuhumiwa kwa makosa mbalimbali ikiwemo kosa la kuchochea vurugu
katika chuo hicho baada ya kutokea mauaji ya Mwanafunzi Henry Koga aliye
uawa kwa kuchomwa kisu juzi akirejea chuoni hapo kutoka kwenye
matembezi yake, hata hivyo haijajulikana mara moja sababu za kuawa kwa
mwanafunzi huyo wala watuhumiwa hawajakamatwa.
Lema: RC amenitumia ujumbe wa vitisho
Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema),
Godbless Lema amedai kupokea ujumbe wa vitisho kwa simu kutoka kwa Mkuu
wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana, Lema alidai kuwa ujumbe huo umeandikwa kupitia simu ambayo namba 0752960276 na unaosomeka: “Umeruka kihunzi cha kwanza, nitakuonesha kuwa mimi ni serikali, ulikojificha nitakupata na nitakupa kesi ninayotaka mimi.”
Alisema baada ya kupata ujumbe huo, alimjibu kuwa “nimekupata nimekuelewa nipo tayari kwa lolote.”
Hata hivyo, Mulongo amekana kumtumia Lema ujumbe
huo... “Nimepata hizi taarifa wewe ni kama mtu wa nane kuniuliza.
Sijatuma huo ujumbe na siwezi kuwa na mawazo ya kumtumia ujumbe huo
kwani kama ningetaka kumkamata tangu jana pale Chuo cha Uhasibu
ningemkamata.”
Hata hivyo, alihoji sababu za mbunge huyo kujificha kama anajijua kwamba hana kosa. “Kwanza nani kamwambia anataka kukamatwa? Yeye anatakiwa kusaidia polisi, kwani wale vijana 13 waliokamatwa kwa ajili yake wapo mahabusu anasubiriwa atoe maelezo.”
kuwa na mawazo ya kumtumia ujumbe huo kwani kama ningetaka kumkamata tangu jana pale Chuo cha Uhasibu ningemkamata.”
Hata hivyo, alihoji sababu za mbunge huyo kujificha kama anajijua kwamba hana kosa. “Kwanza nani kamwambia anataka kukamatwa? Yeye anatakiwa kusaidia polisi, kwani wale vijana 13 waliokamatwa kwa ajili yake wapo mahabusu anasubiriwa atoe maelezo.”
Alisema Mbunge huyo, anajua kazi ambayo, ilifanya
chuo cha uhasibu na ndiyo sababu anajificha... “Alifanya kazi yake
nikazomewa, kama ningetaka kutumia madaraka yangu asingekuwa salama …
nadhani Lema anahitaji kusaidiwa ili abadilike.”
Kuhusu madai ya kujificha, Lema alisema haitajisalimisha polisi licha ya Mulongo kuagiza akamatwe kwa kuwa kuna taratibu za kufuatwa polisi inapomhitaji mbunge ambaye amechaguliwa na watu.
Alisema kama polisi wanamuhitaji, wanapaswa kumuita na pia kuwasiliana na Ofisi ya Spika wa Bunge.
“Naomba ieleweke kuwa mimi sijawakimbia polisi,
siogopi kesi na wala siogopi jela nitaendelea na shughuli zangu waje
kunikamata barabarani,” alisema Lema.
Akizungumzia tukio la juzi, Lema alidai kuwa mkuu huyo wa mkoa ndiye aliyekuwa chanzo cha vurugu kwa kukosa weledi wa kuzungumza na wanafunzi wenye majonzi.
Akizungumzia tukio la juzi, Lema alidai kuwa mkuu huyo wa mkoa ndiye aliyekuwa chanzo cha vurugu kwa kukosa weledi wa kuzungumza na wanafunzi wenye majonzi.
Alisema alikwenda chuoni hapo baada ya kuitwa na
wanafunzi na kabla ya kuzungumza, alikutana na uongozi wa chuo, akiwamo
Kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Arusha.
“OCD Arusha aulizwe kazi ambayo nilifanya kutuliza
hasira za wanafunzi na tutasambaza DVD zaidi ya 3,000 kwa wakazi wa
Arusha kujionea tukio hili ambalo sasa limebadilishwa na kuwa la
kisiasa,” alisema Lema.
Mwanafunzi, Henry Kago(22) aliyeuawa kwa kuchomwa
kisu na watu wasiojulikana na kusababisha wanafunzi kucharuka chuoni
hapo anatarajiwa kusafirishwa leo kwenda Iringa kwa mazishi.
ISOME TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUTOKA KWA MH.LEMA
Jana majira ya saa nne asubuhi nilipokea taarifa kutoka Chuo cha Uhasibu juu ya tukio la mauaji ya mwanafunzi yaliyotokea jana usiku kwa kuchomwa kisu eneo karibu na chuo , nilipita Chuoni hapo baada ya kusikia taarifa hiyo , nilikuta Wanafunzi wengi sana wakiwa wamekusanyika pamoja wakiwa na jazba huku Kamanda wa Jeshi la Polisi Wilaya akijaribu kuwasihi watulie wakati walipokuwa wanatafuta muafaka wa kuzuia jazba ambayo ilikuwa ina lengo la kuandamana kwenda kwa Mkuu wa Mkoa.
Nilipata faragha ya kuongea na Mwalimu aliyekuwa pale ( Dean of Student ) pamoja na OCD na wote walinieleza tatizo lilivyoanza na kuomba nitumie busara kuzuia jazba na maandamano hayo yaliyokuwa yamepangwa kuelekea kwa Mkuu wa Mkoa niliongea na wanafunzi na niliwasihi watulie na nilifanya jitihada za kumtafuta Mkuu wa Wilaya na Mkuu wa Mkoa na kwa bahati nzuri nilimpata Mkuu wa Mkoa na kumweleza juu ya kifo hicho na kile ambacho wanafunzi wanakusudia kufanya kuandamana kwenda ofisini kwake. Nilimuomba afike ili aweze kutuliza hali hile na pia atoe kauli juu ya tukio hilo baya la kuhuzunisha kwani ikizingatiwa kuwa ni zaidi ya mara moja matendo kama haya yamekuwa yakitokea na hakuna hatua zozote zimekuwa zikichukuliwa kuwahakikishia Wanafunzi Usalama wao na mali zao.
Mkuu wa Mkoa pamoja na mimi kumpa taarifa mapema aliahidi kufika mapema jambo ambalo halikufanyika na wanafunzi walianza kuwa wakali na nilifanya jitihada na hekima za hali ya juu kuvuta subira za wanafunzi hao ili Mkuu wa Mkoa afike . Baada ya Mkuu wa Mkoa kufika Makamu wa Chuo aliniomba niwaandae wanafunzi kumsikiliza Mkuu wa Mkoa na yeye alikwenda kumchukua Mkuu wa Mkoa na kumpa mukutasari wa tukio zima na hali halisi ya kilichokuwa kinaendelea na kimsingi Mkuu wa Mkoa alipofika Wanafunzi walitaka apande juu kuongea mahali ambako tulitumia kama jukwaa kwa maongezi wakati wote lakini badala yake mambo yafuatayo yalianza kutokea
1) Mkuu wa Mkoa alikataa na kunitaka nishuke chini mahali alipokuwa yeye na timu yake ya ulinzi na usalama Mkoa kwa kweli nilitii na nilipotaka kuongea nae alinidharau na kuniambia hawezi kuongea na wanafunzi wahuni wasiokuwa na nidhamu maneno ambayo yaliwatia wanafunzi hasira zaidi na nilimsihi na kumuomba Mkuu wa Usalama wa Taifa Mkoa (RSO) kumshawishi Mkuu wa Mkoa kukubali kuongea nao kwani hali ilivyokuwa ni dhahiri kwamba wanafunzi wale walikuwa na jazba ya hali ya juu na hivyo hekima na unyenyekevu ndio ilikuwa njia pekee ya kutuliza hali hile.
2) Mkuu wa Mkoa alitoa masharti kwamba asingeweza kuongea nao bila kipaza sauti na wanafunzi wote waende jengo lililokuwa karibu na Utawala na wakisha kaa atakuja kuongea nao jambo ambalo wanafunzi waligoma kwa imani kwamba jengo hilo lisengeweza kuchukua wanafunzi wengi na mimi niliaga naondoka kwenda msibani na wanafunzi waligoma nisiondoke mpaka watakapo sikilizwa na kwa kweli nilitii maombi baada ya kunizuia na kukaa mbele ya gari yangu.
3) Tulipokwenda eneo la kukutania na mara hii ilikuwa ni nje jirani ya jengo la utawala wanafunzi walikusanyika wakimsubiri Mkuu wa Mkoa na kabla hajafika nilitwa na yeye mwenyewe ili tuweke msimamo wa pamoja kama viongozi lakini badala yake alitumia Polisi kunitisha na kuhaidi kuwa nitamtambua kuwa yeye ni Serikali ,tulitofautiana tena nilipokataa hofu hiyo na ghafla tuliamua kwenda eneo la kuongea na wanafunzi na ndipo yafuatyo yalitokea “
Mkuu wa Mkoa wakati anaanza kuongea alianza kusema maneno yafuatayo “ Mnaona hiki Kifua na huu mwili wangu , na hapo ndipo hali ilipochafuka na kuamsha vurugu kubwa kutoka kwa Wanafunzi waliokerwa na kauli yake na Polisi wa walimchukua na tafrani kati ya Polisi na Wanafunzi ikapamba moto hali iliyosababisha mabomu ya machozi kulipuliwa kwa wingi kila kona ya chuo na kila mtu kuanza kukimbia kuangalia usalama wake nikiwemo mimi .
Nimesikiliza Mkutano wake na Waandishi wa Habari na leo nimesoma nakusikiliza vyombo mbali mbali vya habari kwamba ninatafutwa na Polisi kwa amri ya Mkuu wa Mkoa , nimeshangaa sana japo sio kumshangaa Mkuu huyu wa Mkoa kwani ufahamu na uwezo wake naujua ulivyo katika kufikiri na kutatua mambo ya msingi na muhimu , kwa jinsi nilivyomsikia na kumuona alivyokuwa anashughulikia tatizo lile lililotukutanisha jana pale Chuoni , kwa kweli nilishangazwa sana na kuogopa kama hekima ya Mkiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa angeweza kushughulikia tatizo lile kwa namna ile ya Kiburi , Dharau na Majivuno ambayo hakika ilikuwa ni chanzo cha wanafunzi kukataa kumsikiliza na ndipo alipoamua kuondoka huku zomea zomea ikiendelea kushamiri vizuri . Mabomu yalianza kupigwa , wanafunzi walipigwa na kunyang’anywa pesa , simu , na lap top na vitu mbali mbali ambavyo Polisi walikuwa wanaona vina thamani kwao , nilikuwa ninatazama mambo haya huku roho yangu ikiwa inauma sana kwamba wanaopaswa kulinda usalama wa raia na mali zao ghafla waligeuka kuwa vibaka wa kuumiza raia na kupora mali zao .
Ninawapa pole wanafunzi kwa msiba wa rafiki yao na siku ya jana ilikuwa ni siku ya Serikali kutumia busara kurudisha matumaini kwa wanafunzi wale pamoja na raia , lakini badala yake wafiwa walipotaka kudai haki zao za kulindwa , walipigwa , walidhalilishwa na Chuo chao kufungwa bila sababu ya msingi wala kuzingatia mambo muhimu .
Ifahamike kuwa Chuo cha Uhasibu Arusha kina wanafunzi kutoka sehemu mbalimbali za nchi hii, na amri ya mkuu wa mkoa kufunga chuo na kuamuru wanafunzi watawanyike ifikapo saa kumi na mbili jioni , huu ni ukosefu wa upendo , hekima , busara na utu ikizingatiwa kuwa sababu na mchochezi wa vurugu hizi ni Mkuu wa Mkoa kukosa maarifa na hekima.
Nimepokea ujumbe katika simu yangu kutoka kwenye simu yangu ya kiganjani kutoka kwa Mkuu wa Mkoa inayonitishia na kuweka maisha yangu kwenye hali ya hatari na ujumbe huo unasema “ UMERUKA KIHUNZI CHA KWANZA , NITAKUONYESHA KUWA MIMI NI SERIKALI ULIKOJIFICHA NITAKUPATA NA NITAKUPA KESI NINAYOTAKA MIMI “ Mwisho wa kunukuu .
Mwisho, Ninamshukuru kijana aliyerekodi tukio lote kuanzia mwanzo mpaka mwisho na hivi tutanza kusambaza video cd hizo Nchi ili watanzania wajue ukweli na Mh Rais aone utendaji mbovu wa wateule wake na vile nilitake Jeshi la Polisi kufanya kazi kwa kuzingatia sheria , maadili ,taratibu na kanuni za kazi na sio kuendesha Jeshi kwa matakwa ya kisiasa , kufanya hivi ni kuhatarisha usalama na utulivu wa Nchi yetu .
“ Che Guavera alisema “ if you tremble indignation at every injustice then you are a comrade of mine “
Wanafunzi jipeni moyo bado kitambo kidogo Taifa hili litabadilika .
Godbless J Lema ( MP)
25/4/2013.
KUFUATIA KIFO CHA MWANACHUO ALIYEUWAWA JIJINI ARUSHA CHADEMA CHA TOA TAMKO
TAARIFA KWA UMMA
MAUAJI YA MWANACHUO WA CHUO CHA UHASIBU ARUSHA (HENRY KAGO) NA KAULI YA CHAFU YA MKUU WA MKOA WA ARUSHA
Ndugu wanahabari na wakazi wote wa mkoa wa Arusha.Kwanza kabisa, tunapenda kutoa pole za dhati kwa familia, ndugu jamaa, wanachuo na jumuia yote ya chuo cha uhasibu Arusha wa marehemu Henry Kago aliyefariki juzi usiku kwenye tukio la kutisha na kuhuzunisha sana.
Tumesikitishwa na msiba huu na tunawaombea wote Mungu awapatie faraja na utulivu katika kipindi hiki kigumu.
Katika tukio hili, mbunge wa Arusha Mjini Mhe Godbless Lema alijulishwa na kama kiongozi alifika ili kuona namna atakavyoweza kutoa msaada hasa baada ya wanachuo kuonyesha hisia zao kwa vile hawakuona kupata msaada kutoka kwa uongozi wa chuo na serikali kwa ujumla. Hili ni tukio la pili la mauaji ya mwanachuo sambamba na matukio mengi ya wanachuo kuvamiwa na kunyang’anywa mali zao.
Mhe Lema aliwatuliza wanachuo na kuchukua hatua za kumjulisha mkuu wa Mkoa Mhe Mulongo aje na kuzungumza na vijana hawa.
Hata hivyo ujio wa mhe Mulongo ulionekana haukuwa na dhamira ya dhati na badala yake alionyesha madharau makubwa ambayo mpaka sasa nashindwa kuelewa alikuwa na maana gani kuonyesha tabia ya kipuuzi namna ile kwa vijana waliokuwa wamepata msiba wa mwenzao.
Picha za video zinaonyesha kwa dhahiri jitihada kubwa aliyoifanya mhe Lema kuwatuliza vijana hawa na kuwaomba wawe wavumilivu.
Baada ya tukio zima kukumbwa na vurugu ambazo kimsingi chanzo ni tabia aliyoinyesha Mhe mulongo kwa vijana hawa, mkuu wa mkoa aliongea na waandishi wa habari kuwa chanzo cha vurugu hizo ni Mhe Lema na kuwa tukio zima la mauaji haya ni masuala ya kisiasa na kuwa wanasiasa wamepanga mambo haya ili kujipatia umaarufu, hii na kauli ya mwendawazimu kabisa.
Katika hatua hii walimkamata Wakili Mhe Albert Msando ambaye pia ni diwani wa CHADEMA na kumchukua kwa mahojiano.
Kwa ujumla msingi wa suala la kumtafuta muuaji wa Henry umepabadilika na kuwa kumtafuta Lema.
Tunataka tuweke kumbukumbu hii kwa wakazi wa Arusha, jambo hili ni mfululizo wa matukio mengi yasiyoonyesha weledi ya Mhe mulongo ambayo amekuwa akifanya na kama chama tunamtakia hivi kikombe kitakopajaa atatambua maana ya nguvu ya umma.
Anaweza kudharau maneno haya, afanye hivyo kwa vile anajisikia kuwa yupo na mamlaka ya kiserikali lakini tunarudia kusema kuwa kamwe hatuwezi kuendelea kuvumilia uongo na akili mbovu za namna hii kuongoza watu wenye akili. Narudia kusema hatutavumilia uongo wa namna hii kuendelea kusemwa halafu familia iliyopoteza mtoto wao mpendwa ikiwa katika masononeko makubwa.
Sasa mhe Mulongo na watu wake wajiandae vema maana tumejiandaa kupambana na watu na/au viongozi ambao tumeshajua ni wapotoshaji na wahuni na wanafanya mambo ya kihuni.
Tunawaomba wakazi wa Arusha wawakatae viongozi wapotoshaji na wahuni, wasiwape ushirikiano wowote ule na sisi tutasimama na wananchi kwa pamoja katika mazingira yote ili kudumisha uongozi bora wenye kujali na kuheshimu raia wote kwa mustakabali wa mkoa wetu kiuchumi na katika kujenga utulivu.
Imetolewa leo tarehe 25 Aprili 2013
Amani Golugwa
KATIBU WA CHADEMA – KANDA YA KASKAZINI.
Subscribe to:
Posts (Atom)