wafuasi wa chadema wakiwa wanasubiria hukumu ya Mbunge wao nje ya mahakama kuu ya Arusha |
Mbunge wa Arusha
Mjini Godbless Lema ameachiwa kwa dhamana ya sh. milioni moja baada ya kushtakiwa kwa makosa ya uchochezi
katika mahakama ya Mkoa wa Arusha huku maandamano yakifanyika katika mitaa ya Jiji la Arusha.
Kesi ya uchochezi dhidi ya Lema imefunguliwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Mkoa wa Arusha na inaendeshwa na Hakimu Devota Msoffe
Kesi ya uchochezi dhidi ya Lema imefunguliwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Mkoa wa Arusha na inaendeshwa na Hakimu Devota Msoffe
Kesi hiyo imeahirishwa mpaka Mei 29 mwaka huu huku Katika
hati ya mashtaka ambayo ipo katika mahakama hiyo inasema kwamba kosa la Lema
ni kutoa maneno yanayodaiwa kuwa ni
uchochezi.
Baada ya hukumu hiyo mashabiki,
wafurukutwa na wanachama wa Chadema wamefanya maandamano makubwa kuelekea
katika ofisi za chama hicho ambazo zipo katika eneo la Ngarenaro mkoani humo.
No comments:
Post a Comment