Monday, April 29, 2013

LEMA AACHIWA KWA DHAMANA


wafuasi wa chadema wakiwa wanasubiria hukumu ya Mbunge wao nje ya mahakama kuu ya Arusha


Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema ameachiwa kwa dhamana ya sh. milioni moja  baada ya kushtakiwa kwa makosa ya uchochezi katika mahakama ya Mkoa wa Arusha huku maandamano yakifanyika  katika mitaa ya Jiji la Arusha.

Kesi ya uchochezi dhidi ya Lema imefunguliwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Mkoa wa Arusha na inaendeshwa na Hakimu Devota Msoffe

Kesi  hiyo imeahirishwa mpaka Mei 29 mwaka huu huku Katika hati ya mashtaka ambayo ipo katika mahakama hiyo inasema kwamba kosa la Lema ni  kutoa maneno yanayodaiwa kuwa ni uchochezi.




Baada ya hukumu hiyo mashabiki, wafurukutwa na wanachama wa Chadema wamefanya maandamano makubwa kuelekea katika ofisi za chama hicho ambazo zipo katika eneo la Ngarenaro mkoani humo.

No comments:

Post a Comment