wachezaji wa cap verde wakifanya mazoezi kabla ya mechi ya ufunguzi |
Saturday, January 19, 2013
HII NDIO YANGA BWANA - HIVI NDIVYO ILIVYOWATANDIKA WASAUZI TAIFA LEO
Didier
Kavumbagu (kushoto) akijaribu kumtoka beki wa Black Leopards, wakati wa
Mchezo huo, uliomalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar
es Salaam.
Wachezaji wa Yanga, wakishangilia bao lililofungwa na Jerry Tegete.
jj
Kikosi
cha Yanga.
Kikosi cha Black Leopards.
Mchezaji
wa Yanga, Kabange Twite (kushoto) akimiliki mpira huku akidhibitiwa na
beki wa Black Leopards, Nkosiabo Xakane, wakati wa mchezo huo.
Mashabiki wa Yanga, wakishangilia bao lililofungwa na Jerry Tegete. (PICHA NA SUFIANI MAFOTO)
YANGA YAICHAPA BLACK LEOPARD YA BONDENI 3-2!
kabange twite akichuana na mchezaji wa black leopards |
WIMBI LA TEGETE KUCHEKA NA NYAVU LAMPA JINA “MTURUKI!”
Vinara wa Ligi Kuu Vodacom, Yanga, ambao
pia ndio Mabingwa wa Soka Afrika Mashariki na Kati, leo wakicheza Mechi
yao ya kwanza tangu warejee kutoka Antalya, Uturuki waliko piga Kambi
ya Mazoezi ya Wiki mbili, wameichapa Black Leopard ya Afrika Kusini Bao
3-2 katika Mechi ya Kimataifa ya Kirafiki iliyochezwa Uwanja wa Taifa
Jijini Dar es Salaam.
hawa ni mashabiki wa yanga |
MAGOLI:
Yanga 3
-Tegete Dakika ya 32 & 73
-Domayo 63
Black Leopard 2
-Khoza Dakika ya 47
-Rodney 89
Nyota wa Mechi hii alikuwa Jerry Teget
aliefungia Yanga Bao 2 akiendeleza wimbi la kufunga aliloanza huko
Uturuki kati Mechi za kujipima nguvu kiasi ambacho Washabiki wa Yanga
wameanza kumpachika Jina ‘Mturuki!’.
KIKOSI cha YANGA:
1.Ally Mustafa 'Barthez'
2.Mbuyu Twite
3.Oscar Joshua
4.Nadir Haroub 'Cannavaro'
5.Kelvin Yondani
6.Athumani Idd 'Chuji'
7.Kabange Twite
8.Frank Domayo
9.Didier Kavumbagu
10.Jerson Tegete
11.Haruna Niyonzima
Akiba:
1.Said Mohamed
2.Godfrey Taita
3.Stephano Mwasika
4.Ladislaus Mbogo
5.Shadrack Nsajigwa
6.Nurdin Bakari
7.Saimon Msuva
8.Omega Seme
9.Said Bahanuzi
10.George Banda
11.David Luhende
12.Rehani Kibingu
13.Nizar Khalfani
14.Juma Abdul
Liverpool kumsaini Mbrazil, Zaha Jumatatu ni Man au Arsenal, Big Sam kwa Pilato!!
Klabu
ya Liverpool iko mbioni kumsaini Chipukizi wa Barazil Philippe Coutinho
huku hatima ya Kinda wa Crystal Palace, Wilfried Zaha, kujulikana
Jumatatu na Meneja wa West Ham, Sam Allardyce, amefunguliwa mashitaka na
FA, Chama cha Soka England, kwa kukiuka Kanuni kufuatia kauli yake
dhidi ya Refa aliechezesha Mechi yao na Manchester United.
Liverpool na Mbrazil
Liverpool wako mbioni kusaini Mchezaji
wao wa Pili katika Dirisha hili la Uhamisho la Mwezi Januari baada ya
kutoa Ofa ya Pauni Milioni 8 kumchukua Kiungo wa Inter Milan Philippe
Coutinho.
Coutinho, Miaka 20, ambae ameichezea
Brazil mara moja na alichukuliwa na Inter Milan akiwa na Miaka 16 tu na
kubaki kwao Brazil kwa Mkopo hadi 2010 ambako ndio alitua Inter Milan na
kucheza Mechi 28 lakini Msimu uliopita alipelekwa Spain kuchezea
Espanyol kwa Mkopo.
Mchezaji mwingine alienunuliwa na
Liverpool hii Januari ni Straika kutoka Chelsea Daniel Sturridge
aliechukuliwa kwa Dau la Pauni Milioni 12.
Zaha
Crystal Palace > Arsenal au Man United
Habari za ndani zimedokeza kuwa Uhamisho
wa Wilfried Zaha wa Crystal Palace kwenda Manchester United au Arsenal
utajulikana mwanzoni mwa Wiki ijayo.
Ingawa Man United ndio inayopewa nafasi
kubwa kumchukua Kinda huyo, hasa baada ya Mtendaji Mkuu wa Klabu hiyo,
David Gill, kukiri kuwa wamekuwa wakimfuatilia, lakini pia Arsenal
wamekuwa wakimwinda.
Hata akiuzwa kwa sasa, Crystal Palace
imekuwa ikisisitiza kipengele cha kubaki na Mchezaji huyo hadi mwishoni
mwa Msimu ili awasaidie kuwapandisha Daraja.
Frazier
Sunderland > Cardiff City
Fraizer Campbell yupo mbioni kukamilisha Uhamisho wa £600,000 kutoka Sunderland kwenda Cardiff City.
Straika huyo wa zamani wa Manchester
United ambae ameichezea England mara moja amekuwa akiandamwa na tatizo
la Goti baada ya kuumia vibaya mara mbili katika Goti hilo hilo moja
ambalo limemfanya kiwango kushuka.
Meneja wa Sunderland, Martin O'Neill,
anategemewa kumnunua Danny Graham kutoka Swansea kwa Pauni Milioni 5 ili
kumbadili Frazier Campbell.
M'Vila
Rennes > QPR
Kiungo huyo wa Klabu ya Rennes ya France
ambae anathaminiwa kwa Pauni Milioni 7 anawindwa na Meneja wa QPR Harry
Redknapp lakini pia zipo Klabu nyingine zinazomwandama.
Akiongea kuhusu Yann M'Vila, Loïc Rémy amesema: "Ningependa aje QPR tuwe pamoja. Nishamwambia hapa ni pazuri."
Sam Allardyce ashitakiwa na FA
Meneja wa West Ham Sam Allardyce
amefunguliwa Mashitaka ya Utovu wa Nidhamu na FA, Chama cha Soka
England, kufuatia kauli yake mara baada ya Timu yake Jumatano iliyopita
kufungwa Bao 1-0 na Manchester United na kutupwa nje ya FA CUP.
Alardyce alidai uamuzi wa kuwanyima
Penati Uwanjani Old Trafford na kuwapa Man United Penati ni sababu ya
kucheza Uwanja wa Nyumbani.
Hata hivyo Penati waliyopewa Man United
ilipaishwa na Straika Wayne Rooney. Allardyce amepewa hadi Januari 23
kujibu Mashitaka hayo.
Penati ambayo West Ham wanaidai ni pale Fulbeki Rafael alipokontroli mpira na Paja na kisha kumgonga Mkononi.
Allardyce alikaririwa akisema: “Unaona
kila mara Old Trafford! Hamna tofauti kati ya kushika kwa Rafael na
Jordan Spence. Ila Spence anachezea West Ham, Timu ya ugenini na Rafael
ni Mchezaji wa nyumbani Old Trafford.”
Taarifa ya FA imesema: “Shitaka hili linahusiana na kuvunjwa kwa Kanuni ya FA E3.”
CHANZO SOKA IN BONGO
VPL: KUANZA JANUARI 26, KUWEPO ‘SUPER WEEK ya SUPERSPORT’
UCHAGUZI TFF: 36 WACHUKUA FOMU, 18 WAREJESHA
Mzunguko wa pili ya Ligi Kuu ya Vodacom
utaanza Januari 26 huku kukiwa na maombi ya televisheni ya SuperSport
kuonyesha Mechi za Super Week kama ilivyokuwa katika mzunguko wa kwanza.
KWA TAARIFA ZAIDI:
Release No. 06
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Januari 17, 2013
36 WACHUKUA FOMU TFF, 18 WAREJESHA
Wakati kesho ndiyo mwisho wa kuchukua na
kurejesha fomu za kuwania uongozi kwenye uchaguzi wa Shirikisho la
Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPL Board)
waombaji 36 wameshachukua na 18 tayari wamesharejesha.
Idadi hiyo ni kufikia leo mchana
(Januari 17 mwaka huu). Pia Kamati ya Uchaguzi ya TFF inasisitiza kuwa
wanaorejesha fomu hizo kwa email wanatakiwa kuzituma kwa Katibu Mkuu wa
TFF kwa email ya
tfftz@yahoo.com na si kwa email binafsi za wajumbe wa Kamati ya Uchaguzi au maofisa wa TFF.
Waombaji wanne walioongezeka katika
orodha ni Blassy Kiondo kwa Kanda ya Katavi na Rukwa, Eliud Mvella
(Mbeya na Iringa), Geofrey Nyange (Morogoro na Pwani), na Omari
Abdulkadir kwa Kanda ya Dar es Salaam.
Orodha kamili ya waombaji ni Athuman
Nyamlani, Jamal Malinzi na Omari Mussa Nkwarulo (urais) wakati waombaji
wa umakamu wa rais mpaka sasa ni Michael Wambura, Ramadhan Nassib na
Wallace Karia.
Kwa upande wa wajumbe wa Kamati ya
Utendaji na kanda zao kwenye mabano ni Salum Chama (Kagera na Geita),
Mugisha Galibona, Samuel Nyalla, Titus Osoro na Vedastus Lufano (Mara na
Mwanza).
Epaphra Swai na Mbasha Matutu (Shinyanga
na Simiyu), Charles Mugondo na Elly Mbise (Arusha na Manyara), Yusuph
Kitumbo (Kigoma na Tabora), Ayubu Nyaulingo, Blassy Kiondo, Nazarius
Kilungeja na Selemani Kameya (Katavi na Rukwa) na James Mhagama (Njombe
na Ruvuma).
Athuman Kambi na Zafarani Damoder (Lindi
na Mtwara), Hussein Mwamba na Stewart Masima (Dodoma na Singida), Farid
Nahdi, Geofrey Nyange na Twahili Njoki (Morogoro na Pwani), Elias
Mwanjala na Eliud Mvella (Iringa na Mbeya), Khalid Mohamed (Kilimanjaro
na Tanga) na Muhsin Balhabou, Omari Abdulkadir na Shaffih Dauda (Dar es
Salaam).
Kwa upande wa Bodi ya Ligi Kuu (TPL
Board) waliochukua fomu mpaka sasa ni wawili tu. Yusuf Manji amechukua
fomu ya uenyekiti wakati Said Mohamed amechukua fomu ya kuwania umakamu
mwenyekiti.
SUPER WEEK TENA NDANI YA LIGI KUU YA VODACOM
Mzunguko wa pili ya Ligi Kuu ya Vodacom
utaanza Januari 26 mwaka huu huku kukiwa na maombi ya televisheni ya
SuperSport kuonesha mechi za Super Week kama ilivyokuwa katika mzunguko
wa kwanza.
Raundi tano za awali katika ratiba ya
mzunguko wa pili zinabaki kama zilivyo wakati nyingine zilizobaki
zitatolewa baada ya kuingiza mechi za Super Week.
Wakati huo huo, mzunguko wa pili wa Ligi
Daraja la Kwanza unatarajia kuanza Januari 26 mwaka huu. Ratiba ya ligi
hiyo na tarehe rasmi ya kuanza itatangazwa baada ya kupitiwa na Kamati
ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) inayotarajiwa
kukutana mwishoni mwa wiki.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
VPL: RATIBA:
RAUNDI YA PILI
26 JAN 2013 - 18 MEI 2013
Januari 26
African Lyon v Simba [National Stadium, Dar es Salaam]
Mtibwa Sugar v Polisi Morogoro [Manungu, Morogoro]
Coastal Union v Mgambo JKT [Mkwakwani, Tanga]
Ruvu Shootings v JKT Ruvu [Mabatini, Pwani]
Azam v Kagera Sugar [Azam Complex, Dar es Salaam]
JKT Oljoro v Toto Africans [Sheikh Amri Abeid, Arusha]
Januari 27
Yanga v Tanzania Prisons [National Stadium, Dar es Salaam]
Friday, January 18, 2013
VAN PERSIE ANAVYOIBEBA MAN UNITED...
On Thursday Manchester United boss Sir
Alex Ferguson insisted that his side were not a one-man team and wholly
reliant on hot shot Robin van Persie.
And now he has the stats to back it up
as Sportsmail and Opta can reveal that United have a larger number of
different goalscorers than any other club in the Barclays Premier
League.
United lead the pack with 16 different scorers, ahead of Chelsea and Manchester City who have 14 and 13, respectively.
One man team? Sir Alex Ferguson insists
that Manchester United are not wholly reliant on free-scoring striker
Robin Van Persie (pictured)
Playing their part: Wayne Rooney (left) has seven Premier League goals and Javier Hernandez (right), eight
UNITED'S PL GOALSCORERS
Robin van Persie - 17
Javier Hernandez - 8
Wayne Rooney - 7
Patrice Evra - 4
Jonny Evans - 3
Tom Cleverley - 2
Shinji Kagawa - 2
Rafael - 2
Anderson - 1
Alexander Buttner - 1
Darren Fletcher - 1
Nani -1
Nick Powell - 1
Paul Scholes - 1
Nemanja Vidic - 1
Danny Welbeck - 1
Javier Hernandez - 8
Wayne Rooney - 7
Patrice Evra - 4
Jonny Evans - 3
Tom Cleverley - 2
Shinji Kagawa - 2
Rafael - 2
Anderson - 1
Alexander Buttner - 1
Darren Fletcher - 1
Nani -1
Nick Powell - 1
Paul Scholes - 1
Nemanja Vidic - 1
Danny Welbeck - 1
Liverpool, Spurs and West Ham are adept
at spreading the goals around with 12 each, Norwich have 11, and Reading
and Southampton have ten each.
Arsenal, Everton, Suderland,West Brom
and Wigan will need to show improvement as they have just nine but five
clubs, Aston Villa, Newcastle, QPR, Stoke and Swansea, are at the foot
of the table with only eight different goalscorers.
The importance of Michu to the Swans,
who has 13 of his team's 31 goals is underlined, while Harry Redknapp
will be hoping £8million Loic Remy will bring QPR the goalscoring they
have so desperately needed.
The eight players who have scored for
Redknapp's side only have 17 goals between them, Adel Taarabt leads the
charts with just four.
Though the 29-year-old Dutchman has 21
goals this season, Ferguson is not worried that losing Van Persie would
mean United are a shadow of themselves.
'I don’t go along with the idea we have become a one-man team,' he told United Review.
'There was a time in our history when one man did carry us for a while.
'Eric Cantona kept us in contention with his goals when a few others were off the boil.
'But things are quite different now. Javier Hernandez has weighed in with 12 goals while Wayne Rooney is currently on nine.
'Two defenders, Johnny Evans and Patrice
Evra, have chipped in with eight between them, while opposition players
have gifted three own goals to the league leaders.
'So it doesn’t stand up to see us as a
one-man band overly dependent on Van Persie, brilliant as he has been at
both making and taking goals.'
Spreading the goals: Ferguson's
(pictured) team have 16 different goalscorers in the league this season,
more than any other team
Important goals: Patrice Evra (right) has chipped in with four goals from left-back this season
Ferguson, however, does agree with his
rival Manchester manager, Roberto Mancini, who said that Van Persie is
making the difference this season.
'He is absolutely relishing his new challenge,' he said. 'He is the right player, at the right club, at the right time.
'He has a winning mentality, but as he
points out, it is one that goes right through the squad and one that
will hopefully see us push on in both league and the cups and
successfully navigate what is a busy and challenging period.'
United face Tottenham at White Hart Lane on Sunday.
Thriller: Spurs' Clint Dempsey (pictured) scores the winning goal during the 3-2 thriller at Old Trafford earlier this season
More...
Read more: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-2264478/Manchester-United-man-team.html#ixzz2IKwyMcSz
Follow us: @MailOnline on Twitter | DailyMail on Facebook
WALCOTT AMALIZA MASHAKA ARSENAL, ASAINI MKATABA MPYA HADI 2016 NA MSHAHARA MNONO
Theo Walcott has urged his Arsenal
team-mates to end their eight-year trophy drought after the striker
finally signed a £100,000-a-week deal, keeping him at the club until
2016.
After lengthy negotiations, the England
forward agreed a lucrative three-and-a-half year deal at the Emirates,
including a £3million signing on fee.
The 23-year-old joined fellow young
Britons Jack Wilshere, Kieran Gibbs, Carl Jenkinson, Aaron Ramsey and
Alex Oxlade-Chamberlain, who all signed five-year extensions last
month.
All smiles: Theo Walcott has finally put pen to paper on a new deal at the Emirates
Handy men: Walcott (right) and Arsene Wenger shake on it after the striker signs
After ending any speculation that he
would leave the club, Walcott said: 'I am very happy to have signed a
new contract here at Arsenal.
'Thanks to everyone for their continued support, especially the manager, everyone at the club and most importantly the fans.
'I have made it clear from the start
that I wanted to stay at Arsenal so I am pleased we have agreed a deal
that everyone is happy with.
'What’s important now is for the team to realise its potential and win trophies.'
Arsenal manager Arsene Wenger was delighted to have secured the services of Walcott.
He added: 'Theo is a strong player and
also a great person, and the combination of his ability and pace always
make him such a valuable asset either from the flanks or down the
middle.
'Theo’s contract extension now gives us a
strong nucleus of ambitious young players who have committed to the
Club and want to be successful with us as a group.'
Walcott was expected to agree a deal
sooner, but he baulked at £75,000 per week in August as he held out for a
contract closer to £100,000.
Wenger has seen some of his brightest talents leave the Emirates in the past two summers.
Cesc Fabregas, Samir Nasri, Alex Song
and the Premier League's leading goalscorer this season Robin van Persie
have all departed and the Frenchman was desperate to keep Walcott on
board.
Congratulations: Walcott with team-mates Alex Oxlade-Chamberlain (left) and Wojciech Szczesny (right)
On alert: Arsene Wenger was concerned that another of his prized assets would leave the club
Problem solved: Arsene Wenger managed to convince Walcott to stay at the club
Crisis averted: Samir Nasri (left) moved to Manchester City and Cesc Fabregas (right) left for Barcelona in 2011
The Frenchman had said that he was '99 per cent' certain that Walcott would agree terms before the weekend.
Yesterday, he told The Sun: 'I hope it will be signed before the weekend. There is a possibility. My optimism is at 99 per cent now.'
Walcott joined the Gunners in 2006, when Wenger signed the 16-year-old Southampton academy graduate.
The Englishman is Arsenal's top scorer this campaign with 14 goals in all competitions.
Big loss: Robin van Persie left Arsenal last summer for Manchester United
BRANDTS AIONGOZA YANGA KATIKA MECHI YA 14 LEO
Brandts |
KOCHA Mholanzi,
Ernie Brandts leo anatarajiwa kuiongoza Yanga katika mechi ya 14 tangu ajiunge
nayo Septemba mwaka huu, akitokea APR ya Rwanda wakati itakapomenyana na Black
Leopard ya Afrika Kusini katika mchezo wa kirafiki, Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam.
Yanga SC
iliyorejea wiki Jumapili kutoka Uturuki kwenye kambi ya wiki mbili mjini Antalya,
imekuwa ikijifua katika Uwanja wa Mabatini, Kijitonyama tangu Jumatano kwa
ujumla kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Yanga leo
itakutana na Black Leopard inayoshika nafasi ya 12 katika Ligi Kuu ya Afrika
Kusini yenye timu 16, iliyowasili jana Dar es Salaam ikiwa na msafara wa watu
42 na kufikia katika hoteli ya White Sands, Mbezi Beach, Dar es Salaam.
Wachezaji
wote walifanya mazoezi jana, kasoro kipa wa tatu, Yussuf Abdul na mshambuliaji Hamisi
Kiiza 'Diego' wanaosumbuliwa na Malaria.
Katika mechi
13 ambazo Brandts ameiongoza Yanga hadi sasa tangu arithi mikoba ya Mbelgiji,
Tom Saintfiet, ameshinda saba, kafungwa nne na kutoka sare mbili.
Kati ya
hizo, mechi tisa ni za Ligi Kuu, ambazo amefungwa moja tu dhidi ya Kagera Sugar
mjini Bukoba, wakati nyingine dhidi ya watani wa jadi, Simba SC alitoa sare ya
1-1 na saba ameshinda dhidi ya Toto African 3-1, Ruvu Shooting 3-2, Polisi Moro 3-0, JKT
Oljoro 1-0, JKT Mgambo 3-0, Azam FC 2-0 na Coastal Union 2-0.
Nyingine zote za kirafiki kama ya leo, Yanga walifungwa 1-0
na Tusker Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kabla ya kwenda Uturuki, ambako walianza
kwa sare ya 1-1 Ariminia Bielefed ya Daraja la Nne Ujerumani, kabla ya kufungwa 2-1 na Denizlispor FC ya
Daraja la Kwanza Uturuki na 2-0 na Emmen FC ya Daraja la Kwanza Uholanzi.
REKODI YA
ERNIE BRANDTS YANGA
Yanga 1-1 Simba SC (Ligi
Kuu)
Yanga 0-1 Kagera Sugar (Ligi
Kuu)
Yanga 3-1 Toto African
(Ligi
Kuu)
Yanga 3-2 Ruvu Shooting
(Ligi
Kuu)
Yanga 3-0 Polisi Moro (Ligi
Kuu)
Yanga 1-0 JKT Oljoro (Ligi Kuu)
Yanga 3-0 JKT Mgambo (Ligi
Kuu)
Yanga 2-0 Azam FC (Ligi
Kuu)
Yanga 2-0 Coastal (Ligi
Kuu)
Yanga 0-1 Tusker (Kirafiki)
Yanga 1-1 Ariminia Bielefed (Kirafiki)
Yanga SC 1-2
Denizlispor FC (Kirafiki)
Yanga SC 0-2 Emmen FC (Kirafiki)
Yanga SC Vs
Black Leopard (Kirafiki)SOURCE bIN ZUBERY
AFCON RATIBA NZIMA KWA SAA ZA AFRIKA MASHARIKI
Jumamosi Januari 19
South Africa v Cape Verde Islands [Soccer City Saa 1 Usiku]
Angola v Morocco [Soccer City Saa 4 Usiku]
Jumapili Januari 20
Ghana v Congo DR [Nelson Mandela Bay Stadium Saa 12 Jioni]
Mali v Niger Nelson [Mandela Bay Stadium Saa 3 Usiku]
Jumatatu Januari 21
Zambia v Ethiopia [Mbombela Stadium Saa 12 Jioni]
Nigeria v Burkina Faso [Mbombela Stadium Saa 3 Usiku]
Jumanne Januari 22
Ivory Coast v Togo [Royal Bafokeng Stadium Saa 12 Jioni]
Tunisia v Algeria [Royal Bafokeng Stadium Saa 3 Usiku]
Jumatano Januari 23
South Africa v Angola [Moses Mabhida Stadium Saa 12 Jioni]
Morocco v Cape Verde Islands [Moses Mabhida Stadium Saa 3 Usiku]
Alhamisi Januari 24
Ghana v Mali [Nelson Mandela Bay Stadium Saa 12 Jioni]
Niger v Congo DR [Nelson Mandela Bay Stadium Saa 3 Usiku]
Ijumaa Januari 25
Zambia v Nigeria [Mbombela Stadium Saa 12 Jioni]
Burkina Faso v Ethiopia [Mbombela Stadium Saa 3 Usiku]
Jumamosi Januari 26
Ivory Coast v Tunisia [Royal Bafokeng Stadium Saa 12 Jioni]
Algeria v Togo [Royal Bafokeng Stadium Saa 3 Usiku]
Jumapili Januari 27
Morocco v South Africa [Moses Mabhida Stadium Saa 2 Usiku]
Cape Verde Islands v Angola [Nelson Mandela Bay Stadium Saa 2 Usiku]
Jumatatu Januari 28
Congo DR v Mali [Moses Mabhida Stadium Saa 2 Usiku]
Niger v Ghana [Nelson Mandela Bay Stadium Saa 2 Usiku]
Jumanne Januari 29
Ethiopia v Nigeria [Royal Bafokeng Stadium Saa 2 Usiku]
Burkina Faso v Zambia [Mbombela Stadium Saa 2 Usiku]
Jumatano Januari 30
Algeria v Ivory Coast [Royal Bafokeng Stadium Saa 2 Usiku]
Togo v Tunisia [Mbombela Stadium Saa 2 Usiku]
ROBO FAINALI
Jumamosi Februari 2
Mshindi Kundi B v Mshindi wa Pili Kundi A [Nelson Mandela Bay Stadium Saa 12 Jioni]
Mshindi Kundi A v Mshindi wa Pili Kundi B [Moses Mabhida Stadium Saa 3 na Nusu Usiku]
Jumapili Februari 3
Mshindi Kundi D v Mshindi wa Pili Kundi C [Royal Bafokeng Stadium Saa 12 Jioni]
Mshindi Kundi C v Mshindi wa Pili Kundi D [Mbombela Stadium Saa 3 na Nusu Usiku]
NUSU FAINALI
Jumatano Februari 6
Mshindi RF 3 v Mshindi RF 2 [Mbombela Stadium Saa 12 Jioni]
Mshindi RF 1 v Mshindi RF 4 [Moses Mabhida Stadium Saa 3 na Nusu Usiku]
MSHINDI wa TATU
Jumamosi Februari 9
[Nelson Mandela Bay Stadium Saa 3 Usiku]
FAINALI
Jumapili Februari 10
[Soccer City Saa 3 Usiku]
WANAUME WA AFRIKA WALIOIBUKA MABINGWA KUANZIA MWAKA 1957 MPAKA 2012.
MABINGWA WALIOPITA:
[Kwenye Mabano Nchi Wenyeji]
1957 (Sudan) Egypt 4 Ethiopia 0
1959 (Egypt) Egypt 2 Sudan 1
1962 (Ethiopia) Ethiopia 4 Egypt 2
1963 (Ghana) Ghana 3 Sudan 0
1965 (Tunisia) Ghana 3 Tunisia 2
1968 (Ethiopia) DR Congo 1 Ghana 0
1970 (Sudan) Sudan 1 Ghana 0
1972 (Cameroon) Congo 1 Mali 0
1974 (Egypt) Zaire 2 Zambia 0
1976 (Ethiopia) Morocco
1978 (Ghana) Ghana 2 Uganda 0
1980 (Nigeria) Nigeria 3 Algeria 0
1982 (Libya) Ghana 1 Libya 1 (Ghana-Penati 7-6)
1984 (Ivory Coast) Cameroon 3 Nigeria 1
1986 (Egypt) Egypt 0 Cameroon 0 (Egypt-Penati 5-4)
1988 (Morocco) Cameroon 1 Nigeria 0
1990 (Algeria) Algeria 1 Nigeria 0
1992 (Senegal) Ivory Coast 0 Ghana 0 (Ivory Coast-Penati 11-10)
1994 (Tunisia) Nigeria 2 Zambia 1
1996 (South Africa) South Africa 2 Tunisia 0
1998 (Burkina Faso) Egypt 2 South Africa 0
2000 (Ghana and Nigeria) Cameroon 2 Nigeria 2 (Cameroon-Penati 4-3)
2002 (Mali) Cameroon 0 Senegal 0 (Cameroon-Penati 3-2)
2004 (Tunisia) Tunisia 2 Morocco 1
2006 (Egypt) Egypt 0 Ivory Coast 0 (Egypt-Penati 3-2)
2008 (Ghana) Egypt 1 Cameroon 0
2010 (Angola) Egypt 1 Ghana 0
2012 (Gabon na Equatorial Guinea) Zambia 0 Ivory Coast 0 (Zambia-Penati 8-7)
TATHMINI YA KUNDI kwa KUNDI!
Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON 2013,
yanaanza huko Nchini Afrika Kusini Jumamosi Januari 19 kwa Mechi ya
ufunguzi ya Kundi A kati ya Wenyeji Afrika Kusini na Cape Verde kwenye
Uwanja wa Taifa Mjini Johannesburg.
IFUATAYO NI TATHMINI YA KILA KUNDI:
**FAHAMU: KILA KUNDI LITATOA TIMU 2 KUTINGA ROBO FAINALI.
KUNDI A:
-Afrika Kusini
-Cape Verde
-Morocco
-Angola
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
Wenyeji Afrika Kusini, wakishiriki
Fainali zao za 8, wametwaa Ubingwa wa Afrika mara moja tu pale Mwaka
1996 walipokuwa pia Wenyeji wa Fainali hizo ambako kwenye Fainali
yenyewe waliyotwaa Ubingwa waliichapa Tunisia Bao 2-0 Bao zote
zikifungwa na Mark Williams ambae aliwahi kuichezea Wolverhampton
Wanderers ya England.
Safari hii, Afrika Kusini, maarufu kama
Bafana Bafana, watacheza bila ya Staa wa Everton Stephen Pienaar ambae
alistaafu kuichezea Nchi yake Miezi mitatu iliyopita.
Katika Kundi hili, mpinzani mkubwa wa
Bafana Bafana anaonekana kuwa Morocco ambao walikuwa Washindi wa Pili wa
AFCON 2004 na ambao chini ya Kocha Rachid Taoussi wanaonekana kuimarika
huku Uwanjani wakiwategemea Maprofeshenali kadhaa wanaocheza Klabu
kubwa Ulaya wakiwemo Karim El Ahmadi wa Aston Villa, Beki wa Udinese
Mehdi Benatia na Mchezaji wa Fiorentina, Mounir El Hamadaoui.
Cape Verde, Timu changa inayoshiriki
Fainali zao za kwanza kwa kuwabwaga Vigogo Cameroun 3-2 kwenye mchujo,
wana Wachezaji kadhaa wanaocheza huko Ureno lakini tegemezi kubwa ni
Winga Ryan Mendes, Miaka 22, ambae alifunga Bao 3 kwenye Mechi za Mchujo
za AFCON 2013 na ambae aling’ara huko Ufaransa na Klabu ya Le Havre na kuzolewa na Klabu kubwa Lille Mwaka 2012.
Timu ya 4 ya Kundi A ni Angola ambao
mara mbili wametinga Robo Fainali za AFCON na kuishia hapo na mashine
yao ya Magoli ni Straika wa zamani wa Manchester United, Manucho, ambae
ana rekodi ya kufunga Bao 21 kwa Mechi 38 za Angola.
Manucho anazo Bao 6 kwa Klabu yake ya
sasa ya Spain, Real Valladolid, zikiwamo Bao 2 alizoipiga Real Madrid
walipokutana Mwezi uliopita.
KUNDI B:
-Ghana
-DR Congo
-Niger
-Mali
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
Bila shaka Ghana, moja ya Timu inayopewa nafasi kubwa kutwaa AFCON 2013,
ndio wanaopewa nafasi kubwa kuwa Nambari Wani kwenye Kundi hili na
wamesheheni Majina makubwa kama kina Asamoah Gyan, John Pantsil na John
Mensah lakini pia watawakosa Mastaa wengine, kina Michael Essien, Sulley
Muntari na Andre Ayew, ambao wamefyekwa toka Kikosini na Kocha James
Kwesi Appiah.
Mali na Congo DR ndizo zinazotegemewa
kuchuana ili kupata nafasi moja kuungana na Ghana kwenye Robo Fainali na
zote zina Mastaa maarufu huku Mali ikiwa nao Modibo Maiga wa West Ham
na Samba Diakite wa QPR lakini watamkosa Nahodha wao wa zamani Mahamadou
Diarra anaechezea Fulham kwa kuumia.
Hata hivyo, Mali wanae tena Mchezaji
Momo Sissoko, aliewahi kuichezea Liverpool na sasa yuko Juventus, baada
ya kutoichezea Mali kwa Miaka miwili.
Congo DR nao wana Mastaa wao lakini
atakaebeba jahazi ni Nahodha Tresor Mputu ambae aliwahi kufungiwa Miezi
12 wakati akiechezea Congo kwa kumpiga Refa.
Niger ni Timu ya 4 kwenye Kundi hili na
hii ni Fainali yao ya pili kucheza baada ya AFCON 2012 ambayo hawakuvuka
hatua ya Makundi na safari hii tena wanakadiriwa kufanya hivyo hivyo.
KUNDI C:
-Zambia
-Ethiopia
-Nigeria
-Burkina Faso
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
Kimaandishi, Nigeria wanaonekana kuwa
juu kwenye Kundi hili lakini ukweli ni kuwa Kundi hili liko wazi na
yeyote ana nafasi ya kusonga.
Nigeria wametinga Fainali za AFCON mara 6
lakini wamechukua Ubingwa mara mbili tu na baada ya kuzikosa AFCON 2012
Nchi hiyo ilimteua Mchezaji wao wa zamani, Stephen Keshi kuwa Kocha.
Keshi ameteua Kikosi mchanganyiko cha
Vijana wanaocheza Soka nyumbani na Maprofeshenali kama kina John Mikel
Obi na Victor Moses wa Chelsea na Beki wa zamani wa Everton, Joseph
Yobo.
Zambia ndio Mabingwa watetezi wa Afrika
baada ya kutwaa Taji la AFCON 2012 kwa kuichapa Timu kali Ivory Coast
kwa Mikwaju ya Penati 8-7 huko Nchini Gabon na pia wametinga Fainali
hizi za AFCON 2013 kwa Mikwaju ya Penati walipoitoa Uganda katika Mechi ya mwisho ya Mchujo.
Tegemezi la Zambia ni pamoja na Mchezaji
wa Southampton, Emmanuel Mayuka, Miaka 21, ambae ameichezea Klabu hiyo
ya England Mechi 8, 6 akitokea Benchi.
Timu nyingine za Kundi hili ni Ethiopia
na Burkina Faso lakini Ethiopia washawahi kuwa Mabingwa wa Afrika mara
moja walipotwaa Taji Mwaka 1962 na safari hii Penati ya Dakika ya mwisho
ya Mchezaji Adane Girma kwenye Mechi ya mwisho ya Mchujo na Benin ndio
imewaingiza Fainali za AFCON 2013.
Matokeo mazuri kwa Burkina Faso kwenye Mashindano haya ya Afrika ni kukamata nafasi ya 4 kwenye Fainali za Mwaka 1998.
KUNDI D
-Ivory Coast
-Togo
-Tunisia
-Algeria
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
Wanasema hili ndio ‘Kundi la Kifo!’
Lakini Timu ngumu Ivory Coast,
iliyosheheni Masupastaa wa kila aina, watataka kufanya vyema kupita
AFCON 2012 ambako walitolewa kwenye Fainali na Zambia kwa Matuta 8-7 na
safari hii kutwaa Ubingwa wa Afrika kwa mara ya Pili katika historia
yao.
Macho yote yatakuwa kwa Supa Straika
Didier Drogba, ambae licha ya mafanikio yake makubwa kwenye anga la
Soka, hajawahi kutwaa Ubingwa wa Afrika.
Togo wanatinga kwenye AFCON 2013 wakiwa
na habari njema baada ya Nahodha wao Emmanuel Adebayor kufuta msimamo
wa kususa kuichezea Nchi yake baada ya Rais wa Nchi hiyo kufanya
mazungumzo nae.
Wengine kwenye Kundi hili gumu ni
Algeria na Tunisia ambao kila mmoja ashawahi kuwa Bingwa wa Afrika mara
moja na Timu zote zina Wachezaji kadhaa ambao wako Ulaya.
Algeria wanatawategemea Kiungo wa
Valencia Sofiane Feghouli, Winga wa zamani wa Fulham na Watford, Hamed
Bouazza na Staa wa Nottingham Forest, Guedioura.
Nae Kocha wa Tunisia, Sami Trabelsi,
licha ya kuwa na Mastaa kadhaa, inaelekea amejitia kitanzi mwenyewe
baada ya kumtema Kiungo Nyota wa Atletico Madrid Kader Oueslati na hili
huenda likamfanya atimuliwe ikiwa hatafanikiwa kwani Tunisia, ndani ya
Miaka minne, washabadilisha Makocha mara 7.
AFCON 2013: KABUMBU LINAANZA JUMAMOSI!!
>>AFCON 2013: DONDOO MUHIMU KWA KILA TIMU
AFCON 2013, Mashindano ya kusaka Taifa Bingwa Afrika, yanaanza Jumamosi Januari 19 huko Afrika Kusini na Nchi 16 zinawania Taji hilo.
DONDOO MUHIMU ZA KILA NCHI-VIKOSI/MAMENEJA/REKODI:
KUNDI A
South Africa
JINA MAARUFU: Bafana Bafana
UBORA FIFA: 87
RANGI: Kijani na Dhahabu
REKODI BORA AFCON: Mabingwa 1996
MENEJA: Gordon Igesund
Miaka 56– Ni Gwiji wa Soka Nchini Afrika Kusini baada ya kuwahi kuwa
Meneja wa Klabu 7 Nchini humo. Alicheza Soka lake Nchini Austria na
kuteuliwa Meneja Juni 2012.
NAHODHA: Bongani
Khumalo – Baada ya kustaafu Mchezaji wa Everton Steven Pienaar, Bongani
Khumalo ndie akapewa Unahodha. Ni Mchezaji wa Tottenham lakini yupo kwa
Mkopo huko Ugiriki na Klabu ya PAOK.
NYOTA: Katlego Mphela –
Ameichezea Bafana Bafana tangu 2005 na kufunga Bao 23 katika Mechi 47
appearances na Bao lake la kukumbukwa ni lile la Mashindano ya FIFA ya
Kombe la Mabara Mwaka 2009 alipopiga Frikiki tamu iliyoipeleka Mechi ya
kutafuta Mshindi wa 3 na Spain kwenye Dakika 30 za Nyongeza.
KIKOSI:
MAKIPA: Itumeleng Khune (Kaizer Chiefs), Senzo Meyiwa (Orlando Pirates), Wayne Sandilands (Mamelodi Sundowns)
MABEKI: Siboniso Gaxa
naTshepo Masilela (Chiefs), Thabo Matlaba and Siyabonga Sangweni
(Pirates), Bongani Khumalo (PAOK), Anele Ngcongca (Genk), Thabo Nthethe
(Bloemfontein Celtic)
VIUNGO: Reneilwe
Letsholonyane na Siphiwe Tshabalala (Chiefs), Lerato Chabangu (Moroka
Swallows), Kagiso Dikgacoi (Crystal Palace), Dean Furman (Oldham), Max
Mahlangu (Helsingborg), Oupa Manyisa (Pirates), Thuso Phala (Platinum
Stars), Thulani Serero (Ajax)
MASTRAIKA: Lehlohonolo Majoro na Bernard Parker (Chiefs), Katlego Mphela (Sundowns), Tokelo Rantie (Malmo)
Morocco
JINA MAARUFU: Lions of the Atlas
UBORA FIFA: 74
RANGI: Nyekundu
REKODI BORA AFCON: Mabingwa 1976
MENEJA: Rachid Taoussi –
Ni Meneja mpya aliembadili Eric Gerets baada ya Morocco kuaibishwa na
Mozambique katika Mechi ya Kwanza ya Mchujo ya AFCON 2013 walipochapwa
2-0 lakini yeye akaisaidia Morocco kushinda 4-0 katika Mechi ya
Marudiano. Taoussi, Miaka 56, alijijengea sifa baada ya kuiwezesha Klabu
ya Morocco Maghreb Fez kutwaa Mataji matatu ya CAF Kombe la Shirikisho,
African Super Cup na Throne Cup.
NAHODHA: Nadir Lamyaghri –Ni Kipa wa muda mrefu wa Morocco.
NYOTA: Abdelaziz Barrada – Ni Kijana wa Miaka 23 Kiungo anaechezea La Liga na Klabu ya Getafe.
KIKOSI:
MAKIPA: Khalid Askiri (Raja Casablanca), Nadir Lamyaghri (Wydad Casablanca), Anas Zniti (Moghreb Fes)
MABEKI: Abderahim
Chakir (FAR Rabat), Abdelatif Nousseir (Moghreb Fes), Issam El Adoua
(Guimaraes), Mehdi Benatia (Udinese), Zakarya Bergdich (Lens), Ahmed
Kantari (Brest), Abdelhamid El Kaoutari (Montpellier)
VIUNGO: Karim El Ahmadi
(Aston Villa), Abdelaziz Barrada (Getafe), Chahir Belghazouani
(Ajaccio), Younes Belhanda (Montpellier), Adil Hermach (Al Hilal), Kamal
Chafni (Brest), Mehdi Namli (Moghreb Tetouan)
MASTRAIKA: Nordin
Amrabat (Galatasaray), Youssef El Arabi (Granada), Oussama Assaidi
(Liverpool), Abderrazak Hamdallah (Olympique Safi), Mounir El Hamdaoui
(Fiorentina), Youssef Kadioui (FAR)
Angola
JINA MAARUFU: The Sable Antelopes
UBORA FIFA: 84
RANGI: Nyekundu na Nyeusi
REKODI BORA AFCON: Robo Fainali 2008 na 2010
MENEJA: Gustavo Ferrin – Ni Raia wa Uruguay.
NAHODHA: Manucho – Ni Mchezaji wa zamani wa Manchester United ambae sasa yupo Real Valladolid ya Spain.
NYOTA: Djalma Campos – Ni Fowadi anachezea FC Porto ingawa yuko kwa Mkopo kwa Kasimpasa ya Turkey.
KIKOSI:
MAKIPA: Lama (Petro Atletico), Landu (Recreativo Libolo), Neblu (Primeiro Agosto)
MABEKI: Amaro, Bastos
and Dani Massunguna (Primeiro), Fabricio, Mingo Bille na Pirolito
(InterClube), Marco Airosa (AEL Limassol), Lunguinha (Kabuscorp), Zuela
(Apoel Nicosia)
VIUNGO: Dede and Gilberto (AEL Limassol), Manucho Dinis (Primeiro), Manuel (Aviacao), Miguel (Petro)
MASTRAIKA: Djalma
(Kasimpasa), Geraldo (Parana), Guilherme Afonso (Vaduz), Manucho
Goncalves (Real Valladolid), Mateus (Nacional), Yano (Progresso)
Cape Verde Islands
JINA MAARUFU: Blue Sharks
UBORA FIFA: 69
RANGI: Bluu, Nyeupe na Nyekundu
REKODI BORA AFCON: Mashindano yao ya kwanza
MENEJA: Lucio Antunes –
NAHODHA: Nando Maria
Neves – Ni Sentahafu mwenye Miaka 34 anaechezea Klabu ya Daraja la Pili
Chateauroux ya France ingawa ashacheza Soka Nchini Portugal,
Switzerland, Tunisia, Qatar na Czech Republic.
NYOTA: Ryan Mendes – Ni Chipukizi wa Miaka 23 anaecheza huko France Klabuni Lille.
KIKOSI:
MAKIPA: Fock (Petro Atletico), Rilly (Mindelense), Vozinha (Progresso Sambizanga)
MABEKI: Carlitos (AEL
Limassol), Fernando Varela (Vaslui), Gege (Maritimo), Guy Ramos
(Waalwijk), Josimar (Dordrecht), Nando (Chateauroux), Nivaldo (Academica
Coimbra), Pecks (Gil Vicente)
VIUNGO: Babanco and
David Silva (Olhanense), Platini (Santa Clara), Roni (Fola Esch), Marco
Soares (Omonia Nicosia), Stenio (Feirense), Toni Varela (Sparta
Rotterdam)
MASTRAIKA: Djaniny (Olhanense), Heldon (Maritimo), Julio Tavares (Dijon), Ryan Mendes (Lille), Rambe (Belenenses)
KUNDI B
Ghana
JINA MAARUFU: Black Stars
UBORA FIFA: 30
RANGI: Nyeupe
REKODI BORA AFCON: Mabingwa 1963, 1965, 1978, 1982
MENEJA: James Kwesi
Appiah – Baada ya kuwa na Mameneja wawili kutoka Serbia Ghana iliamua
kumteua Mzalendo na huyo ni Mtumishi wa muda mrefu wa Ghana akiwa
Nahodha wa Ghana kuanzia 1987 hadi 1992.
NAHODHA: Asamoah Gyan –
Ana historia ya kupanda na kushuka kwa Nchi yake Ghana baada ya
kuifungia Magoli muhimu likiwemo lile la ushindi dhidi ya USA katika
Mechi ya Raundi ya Pili ya Kombe la Dunia Mwaka 2010 kwenye muda wa
Nyongeza lakini pia alikosa Penati dhidi ya Uruguay baada ya Luis Suarez
kuudaka mpira katika Robo Fainali ya Kombe la Dunia Mwaka 2010.
Gyan sasa anachezea Klabu ya UAE, Falme za Nchi za Kiarabu, Al Ain.
KIKOSI:
MAKIPA: Daniel Adjei (Liberty Professionals), Fatau Dauda (Ashanti Gold), Adam Kwarasey (Stromsgodset)
MABEKI: Harrison Afful
(Esperance), Jerry Akaminko (Eskisehirspor), Mohammed Awal (Maritzburg
Utd), John Boye (Rennes), Kissi Boateng (Berekum Chelsea), Jonathan
Mensah (Evian), John Paintsil (Hapoel Tel Aviv), Isaac Vorsah (Red Bull
Salzburg)
VIUNGO: Albert Adomah
(Bristol City), Anthony Annan (Osasuna), Kwadwo Asamoah (Juventus),
Solomon Asante (Berekum), Christian Atsu (Porto), Emmanuel Agyemang Badu
(Udinese), Derek Boateng (Dnipro Dnipropetrovsk), Mohammed Rabiu
(Evian), Mubarak Wakaso (Espanyol)
MASTRAIKA: Emmanuel Clottey (Esperance), Asamoah Gyan (Al Ain), Richmond Boakye Yiadom (Sassuolo)
NYOTA: Kwadwo Asamoah – Ana Umri wa Miaka 24 na ni Mchezaji wa Mabingwa Italy, Juventus.
Congo DR
JINA MAARUFU: The Leopards
UBORA FIFA: 99
RANGI: Bluu na Nyekundu
REKODI BORA AFCON: Mabingwa 1968 na 1974
MENEJA: Claude Le Roy – Ni Mfaransa ingawa imeripotiwa amebwaga manyanga kuifundisha Congo, kitu ambacho amekikanusha.
NAHODHA: Tresor Mputu – Ni Mchezaji wa Miaka 27 ambae ni Mfungaji hatari.
KIKOSI:
MAKIPA: Robert Kidiaba (TP Mazembe), Bakala Landu (MK Etancheite), Parfait Mandanda (Charleroi)
MABEKI: Jean Kasusula
(Mazembe), Larrys Mabiala (Karabukspor), Chancel Mbemba (Anderlecht),
Cedric Mongongu (Evian), Issama Mpeko (Vita Club), Landry Mulemo
(Kortrijk), Gabriel Zakuani (Peterborough)
VIUNGO: Dioko
Kaluyituka (Al-Kharitiyath), Deo Kanda (Mazembe), Cedric Makiadi
(Freiburg), Zola Matumona (Mons-Bergen), Tresor Mputu (Mazembe),
Youssouf Mulumbu (West Bromwich Albion)
MASTRAIKA:
Patou Kabangu (Mazembe), Yves Diba (Al-Raed), Domi Kumbela (Eintracht
Brunswick), Tresor LuaLua Lomana (Karabukspor), Manzia Budje (Shark),
Dieumerci Mbokani (Anderlecht), Luvumbu Nzinga (Rojolu)
Mali
JINA MAARUFU: The Eagles
UBORA FIFA: 25
RANGI: Njano, Nyekundu na Kijani
REKODI BORA AFCON: Washindi wa Pili 1972
MENEJA: Patrice Carteron
NAHODHA: Seydou Keita
Aliichezea Barcelona kwa Miaka minne hadi Msimu uliopita na kutwaa
Ubingwa wa La Liga mara 3 na Ubingwa wa Ulaya mara 2.
KIKOSI:
MAKIPA: Soumbeyla Diakite (Stade Malien), Mamadou Samassa (Guingamp), Aly Yirango (Djoliba)
MABEKI: Adama Coulibaly
(Auxerre), Idrissa Coulibaly (Lekihwiya), Ousmane Coulibaly (Brest),
Salif Coulibaly (Djoliba), Fousseyni Diawara (Ajaccio), Mahamadou Ndiaye
(Vitoria Guimaraes), Adama Tamboura (Randers), Molla Wague (Caen)
VIUNGO: Samba Diakite
(QPR), Cheick Fantamady Diarra (Rennes), Sigamary Diarra (Ajaccio),
Seydou Keita (Aerbin Dalian), Mohamed Lamine Sissoko (Paris Saint
Germain), Samba Sow (Lens), Kalilou Traore (Sochaux), Mahamane Traore
(Nice), Sambou Yatabare (Bastia)
MASTRAIKA: Cheick Tidiane Diabate (Bordeaux), Modibo Maiga (West Ham), Mamadou Samassa (Chievo)
NYOTA: Modibo Maiga – Ni hatari kwa ufungaji lakini hatabiriki.
Niger
JINA MAARUFU: Gazelles
UBORA FIFA: 105
RANGI: Nyeupe
REKODI BORA AFCON: Raundi ya Kwanza 2012
MENEJA: Gernot Rohr – Ni Mjerumani mwenye Miaka 59.
NAHODHA: Moussa Maazou – Ni Mchezaji wa Miaka 28 anaechezea Klabu ya Tunisia, Etoile du Sahel.
KIKOSI:
MAKIPA: Moussa Alzouma (Garde Nationale), Daouda Kassaly (Chippa Utd), Saminou Rabo (Sahel)
MABEKI: Ismael
Alassane, Kader Amadou na Mohamed Soumaila (Olympic), Mohamed Bachar and
Luky James (AS Douane), Mohammed Chikoto (Marsa), Koffi Dankowa
(Zarzis), Kourouma Fatogoma (Chabab)
VIUNGO: Issoufou
Boubacar (clubless), Karim Konate (clubless), Issiakou Koudize (Garde
Nationale), Idrissa Laouali (Mangasport), Amadou Mountari (Le Mans),
Williams N’Gonou (LB 07), Souleymane Sakou (Olympic), Babacar Talatou
(AmaZulu)
MASTRAIKA: Kamilou Daouda (Saoura), Issoufou Dante (Wydad Fes), Moussa Maazou (Etoile Sahel), Modibo Sidibé (clubless)
NYOTA: Daouda Kamilou – Ana Umri wa Miaka 25 na yupo Klabu ya Algeria JS Saoura.
KUNDI C
Nigeria
JINA MAARUFU: Super Eagles
UBORA FIFA: 52
RANGI: Kijani
REKODI BORA AFCON: Mabingwa 1980 na 1994
MENEJA: Stephen Keshi –
Ni Nguli wa Soka la Nigeria na ameichezea Nchi yake mara 64 na
aliichukua Nchi yake mara baada ya kushindwa kufuzu kuingia Fainali za
AFCON 2012.
Amewahi pia kuwa Meneja wa Timu za Taifa za Mali na Togo.
NAHODHA: Joseph Yobo –
Ni Sentahafu Veterani aliewahi kuichezea Everton na yupo Timu ya Taifa
ya Nigeria kwa Miaka 12 na kucheza Mechi 89.
Yobo, Miaka 32, anaichezea Fenerbahce ya Turkey.
KIKOSI:
MAKIPA: Chigozie Agbim (Enugu Rangers), Austin Ejide (Hapoel Be’er Sheba), Vincent Enyeama (Maccabi Tel Aviv)
MABEKI: Efe Ambrose
(Celtic), Elderson Echiejile (Braga), Azubuike Egwuekwe (Warri Wolves),
Kenneth Omeruo (ADO Den Haag), Godfrey Oboabona (Sunshine Stars), Juwon
Oshaniwa (Ashdod), Joseph Yobo (Fenerbahce)
VIUNGO: Reuben Gabriel
(Kano Pillars), Nosa Igiebor (Real Betis), John Obi Mikel (Chelsea),
Obiora Nwankwo (Calcio Padova), Fegor Ogude (Valerenga), Ogenyi Onazi
(Lazio)
MASTRAIKA: Sunday Mba
and Ejike Uzoenyi (Enugu), Emmanuel Emenike (Spartak Moscow), Brown
Ideye (Dynamo Kyiv), Victor Moses (Chelsea), Ahmed Musa (CSKA Moscow),
Ikechukwu Uche (Villarreal)
NYOTA: John Obi Mikel - Ana Miaka 25 na yupo Chelsea ambako ameshacheza Mechi 263.
Zambia
JINA MAARUFU: The Copper Bullets [Chipolopolo]
UBORA FIFA: 34
RANGI: Chungwa na Kijani
REKODI BORA AFCON: Mabingwa 2012
MENEJA: Herve Renard –
Sasa ni Shujaa wa Zambia baada ya kuiongoza Nchi hiyo kutwaa Ubingwa wa
Afrika Mwaka jana ambako walizifunga Timu kubwa za Senegal, Ghana na
ivory Coast.
NAHODHA: Christopher Katongo – Ndio Mchezaji Bora wa BBC kwa Mwaka 2012.
KIKOSI:
MAKIPA: Daniel Munyau (Red Arrows), Kennedy Mweene (Free State Stars), Joshua Titima (Power Dynamos)
MABEKI: Hichani
Himoonde, Francis Kasonde and Stoppila Sunzu (TP Mazembe), Emmanuel
Mbola (Porto), Joseph Musonda (Golden Arrows), Davies Nkausu (SuperSport
Utd)
VIUNGO:
Isaac Chansa and Christopher Katongo (Henan Jianje), Rainford Kalaba
and Nathan Sinkala (Mazembe), Noah Chivuta (Free State Stars), Felix
Katongo (Petro Atletico), Chisamba Lungu (Ural Oblast), Mukuka Mulenga
(Power Dynamos), William Njobvu (Hapoel Beer Sheba)
MASTRAIKA: James
Chamanga (Liaojing Whowin), Emmanuel Mayuka (Southampton), Collins
Mbesuma (Orlando Pirates), Jacob Mulenga (Utrecht), Jonas Sakuwaha (Al
Merreikh)
NYOTA: Emmanuel Mayuka – Ndie alietwaa Buti ya Dhahabu AFCON 2012 na sasa yupo na Klabu ya England Southampton.
Ethiopia
JINA MAARUFU: Walya Antelopes or Black Lions
UBORA FIFA: 110
RANGI: Njano na Kijani
REKODI BORA AFCON: Mabngwa 1962
MENEJA: Sewnet Bishaw – Hii ni mara ya pili kwa yeye kuwa Meneja wa Ethiopia.
NAHODHA: Degu Debebe – Ni Sentahafu anaechezea Klabu ya Ethiopia Saint-George.
KIKOSI:
MAKIPA: Sisay Bancha (Dedebit), Zerihun Tadele (St George), Jemal Tassew (Coffee)
MABEKI: Abebaw Butako,
Degu Debebe, Biadgelegn Elias na Alula Girma (St George), Berhanu
Bogale, Aynalem Hailu and Seyoum Tesfaye (Dedebit)
VIUNGO: Behailu Assefa,
Addis Hintsa na Minyahil Teshome (Dedebit), Shimeles Bekele na Yared
Zinabu (St George), Dawit Estifanos (Coffee), Asrat Megersa (EEPCO),
Yusuf Saleh (Syrianska)
MASTRAIKA: Adane Girma and Oumed Ukuri (St George), Fuad Ibrahim (Minnesota Stars), Getaneh Kebede (Dedebit), Saladin Said (Wadi Degla)
NYOTA: Adana Girma – Ni Mchezaji wa Saint-George na hatari kwa Mabao.
Burkina Faso
JINA MAARUFU: The Stallions
UBORA FIFA: 89
RANGI: Kijani
REKODI BORA AFCON: Nafasi ya Nne 1998
MENEJA: Paul Put – Ni Raia wa Belgium.
NAHODHA: Moumouni
Dagano – Ni Mchezaji anaecheza Klabu ya Qatar Al-Sailiya na ndie mmoja
wa Wafungaji Bora wa Mechi za Mchujo za Kombe la Dunia za Mwaka 2010 kwa
kufunga Bao 12.
KIKOSI:
MAKIPA: Daouda Diakite (Lierse), Germain Sanou (St Etienne), Abdoulaye Soulama (Asante Kotoko)
MABEKI: Mohamed Koffi
(Petrojet), Bakary Kone (Lyon), Paul Koulibaly (Dynamo Bucharest), Mady
Panandetiguiri (Antwerp), Henri Traore (Ashanti Gold)
VIUNGO: Charles Kabore
(Marseille), Djakaridja Kone (Evian), Prejuce Nacoulma (Gornik Zabrze),
Issouf Ouattara (Chernomorets Burgas), Jonathan Pitroipa (Rennes), Aly
Rabo (Al Shorta), Florent Rouamba (Sheriff Tiraspol), Wilfried Sanou
(Kyoto Sanga), Abdou Razack Traore (Lechia Gdansk), Alain Traore
(Lorient)
MASTRAIKA: Wilfried Dah
na Pierre Koulibaly (Al Dhaid Sharjah), Wilfried Balima (Sheriff
Tiraspol), Aristide Bance (Augsburg), Moumouni Dagano (Al Siliya)
NYOTA: Alain Traore – Ni Kaka wa Mchezaji mdogo wa Chelsea, Bertrand, ambae anachezea Klabu ya Llorient.
KUNDI D
Ivory Coast
JINA MAARUFU: The Elephants
UBORA FIFA: 14
RANGI: All-orange
REKODI BORA AFCON: Mshindi 1992
MENEJA: Sabri Lamouchi –
Ana Miaka 41, Lamouchi na ni chaguo la ajabu kuiongoza Ivory Coast
baada ya kuwa Mchezaji wa Auxerre, Monaco, Parma, Inter Milan na
Marseille pamoja na Timu ya Taifa ya France aliyoichezea mara 12.
NAHODHA: Didier Drogba –
ndie Mchezaji anaetambulika sana kwa Ivory Coast na mwenye Rekodi safi
ya Mabao kwa Nchi yake, Bao 59 kwa Mechi 90.
Baada ya kuibeba Chelsea kutwaa Ubingwa wa Ulaya Mwaka jana, Drogba sasa yuko China na Klabu ya Shanghai Shenhua.
KIKOSI:
MAKIPA: Boubacar Barry (Lokeren), Daniel Yeboah (Dijon), Ali Badra Sangare (Ivoire Academie)
MABEKI: Souleymane
Bamba (Trazbonspor), Arthur Boka (Stuttgart), Emmanuel Eboue
(Galatasaray), Igor Lolo (Kuban Krasnodar), Siaka Tiene (PSG), Kolo
Toure (Manchester City), Ismael Traore (Brest/FRA)
VIUNGO: Max Gradel
(Saint-Etienne), Didier Ya Konan (Hanover), Abdul Razak (Manchester
City), Romaric Ndri Koffi (Real Zaragoza), Cheick Tiote (Newcastle),
Yaya Toure (Manchester City), Didier Zokora (Trazbonspor)
MASTRAIKA: Wilfried
Bony (Vitesse Arnhem), Didier Drogba (Shanghai Shenhua), Gervinho
(Arsenal), Salomon Kalou (Lille), Arouna Kone (Wigan), Lacina Traore
(Anzhi Makhachkala)
NYOTA: Yaya Toure – Ni Kiungo imara alieichezea Nchi yake mara 72.
Tunisia
JINA MAARUFU: The Eagles of Carthage
UBORA FIFA: 45
RANGI: Nyeupe
REKODI BORA AFCON: Mabingwa 2004
MENEJA: Sami Trabelsi –
Ni Kocha mdogo mwenye Miaka 44 lakini ana uzoefu mkubwa baada ya
kung’ara akiichezea Tunisia kati ya 1994 na 2001.
NAHODHA: Aymen Mathlouthi - Ni kipa mwenye Miaka 28 anaedakia Klabu ya Tunisia Etoile du Sahel na ameichezea Tunisia Mechi 38.
KIKOSI:
MAKIPA: Moez Ben Cherifia (Esperance), Aymen Mathlouthi (Etoile Sahel), Farouk Ben Mustapha (CA Bizertin)
MABEKI: Khalil Chammam
and Walid Hichri (Esperance), Aymen Abdennour (Toulouse), Anis Boussaidi
(Tavria Simferopol), Chamseddine Dhaouadi (Etoile), Fateh Gharbi (CS
Sfaxien), Bilel Ifa (Club Africain)
VIUNGO: Youssef Msakni,
Khaled Mouelhi na Mejdi Traoui (Esperance), Haten Baratli (Club
Africain), Oussama Darragi (Sion), Chadi Hammami (Kuwait SC), Wissem
Yahia (Mersin Idman Yurdu)
MASTRAIKA: Zouheir
Dhaouadi (clubless), Hamdi Harbaoui (Lokeren), Issam Jomaa (Kuwait SC),
Wahbi Khazri (Bastia), Saber Khlifa (Evian), Fakreddine Ben Youssef
(Sfaxien)
NYOTA: Issam Jemaa – Ni
Straika ambae aliwahi kuichezea Auxerre ya France lakini sasa yupo
Nchini Kuwait ambae ameifungia Tunisia Bao 34 katika Mechi 70.
Algeria
JINA MAARUFU: Fennec Foxes, Desert Warriors
UBORA FIFA: 19
RANGI: Nyeupe
REKODI BORA AFCON: Mabingwa 1990
MENEJA: Vahid
Halilhodzic – Ni Kocha kutoka Bosnia ambae ameanza kuifundisha Algeria
tangu Juni 2011 na aliwahi kuipeleka Ivory Coast Fainali za Kombe la
Dunia za Mwaka 2010 lakini akatimuliwa Miezi minne tu kabla Mashindano
hayo kuanza.
NAHODHA: Medhi Lacen – Ni Kiungo anaechezea Getafe ya Spain.
KIKOSI:
MAKIPA: Azzeddine Doukha (Harrach), Rais Mbolhi (Krylia Sovetov), Cedric Si Mohammed (Bejaia)
MABEKI: Essaïd Belkalem
and Ali Rial (JS Kabylie), Carl Medjani and Mehdi Mostefa (Ajaccio),
Liassine Cadamuro (Real Sociedad), Faouzi Ghoulam (Saint-Etienne), Rafik
Halliche (Academica), Djamel Mesbah (AC Milan)
VIUNGO: Hameur Bouazza
(Racing Santander), Ryad Boudebouz (Sochaux), Sofiane Feghouli
(Valencia), Adlene Guedioura (Nottingham Forest), Foued Kadir
(Marseille), Medhi Lacen (Getafe), Khaled Lemmouchia (Club Africain),
Saad Tedjar (USMA)
MASTRAIKA: Mohamed Aoudia (Entente Setif), Yacine Bezzaz (CS Constantine), Islam Slimani (Belouizdad), Hilal Soudani (Guimares)
NYOTA: Sofiane
Feghouli – Ni Chipukizi wa Miaka 23 anaechezea Valencia ya Spain na pia
aliwahi kuchezea Timu za Taifa za Vijana za France kabla kurudi kwenye
Nchi ya asili yake.
Togo
JINA MAARUFU: The Sparrow Hawks
UBORA FIFA: 71
RANGI: Njano
REKODI BORA AFCON: Raundi ya Kwanza 1972, 1984, 1998, 2000, 2002 na 2006
MENEJA: Didier Six – Ameshaichezea Timu ya Taifa ya France kwenye Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 1978 na 1982.
NAHODHA: Emmanuel Adebayor – Ndie nguzo ya Togo ambae ameifungia Bao 26 katika Mechi 54.
KIKOSI:
MAKIPA: Mawugbe Atsou (Maranatha), Baba Tchagouni (Dijon)
MABEKI: Serge Akakpo
(Zilina), Sadat Ouro-Akoriko (Free State Stars), Vincent Bossou
(Navibank), Djene Dakonam (Coton Sport), Donou Kokou (Maranatha),
Abdoul-Gafar Mamah (Dacia), Senah Mango (Marseille), Dare Nibombe
(Boussou Dur Borinage)
VIUNGO: Kodjo Ametepe
(Maranatha), Komlan Amewou (Nimes), Sapol Mani (Batna), Moustapha
Salifou (clubless), Prince Segbefia (Auxerre), Dove Wome (Free State
Stars)
MASTRAIKA: Kalen Damessi (Lille), Thomas Dossevi (Chonburi), Serge Gakpe (Nantes), Fessou Placa (Agaza), Emmanuel Adebayor (Tottenham)
NYOTA: Bila shaka ni Adebayor!
Subscribe to:
Posts (Atom)