|
Yanga: Ally
Mustapha 'Barthez', Stephano Mwasika, Oscar Joshua, Nadir Haroub 'Cannavaro'
(C), Kelvin Yondan, Athuman Idd 'Chuji', Rashid Gumbo, Haruna Niyonzima, Said
Bahanunzi, Hamis Kiiza 'Diego', David Luhende - 29.
Akiba: Yaw
Berko, Ladislaus Mbogo, Juma Seif 'Kijiko', Idrisa Rashid, Shamte Ally, Nizar
Khalfan, Jeryson Tegete
|
Klabu ya
Soka ya Yanga leo kwenye Uwanja wa Taifa
Jijini Dar es Salaam wamefanikiwa kutetea vizuri Taji lao la Klabu Bingwa Afrika ya Mashariki
na ya Kati walipoitandika Timu ngumu ya Azam FC bao 2-0 kwenye Fainali na
kuendelea kubaki na kombe hilo la KAGAME baada ya kulitwaa Mwaka jana walipowafunga
Mahasimu wao wakubwa Simba kwa bao 1-0.
Aidha Wafungaji
wa Yanga leo ni Mastraika wao hatari
sana, Hamisi Kiiza na Said Bahanuzi, ambao ndio walipachika bao za leo na kila
mmoja kufikisha Bao 6 wakifungana na Teddy Etekiama wa Vita Club ya DRC kwa
kuwa ndio Wafungaji Bora wa Mashindano haya.
Bao la
kwanza la Yanga lilifungwa na Hamisi Kiiza katika Dakika ya 44 na Said Bahanuzi
akapiga Bao la pili katika Dakika ya 90.
|
Mwenyekiti mpya wa Yanga, Yusuf Manji.
|
Hakika hii
ni chereko kubwa huko Jangwani kwa Mwenyekiti mpya wa Yanga, Yusuf Manji, na
Kocha wao mpya Tom Saintfient kwani huu ulikuwa ni mtihani wao mkubwa wa kwanza
tangu watwae nyadhifa zao hivi karibuni.
|
Kikosi cha Vita Club ya Congo DR.
|
Katika Mechi
ya awali ya kusaka Mshindi wa Tatu, Vita Club ya Congo DR iliifunga APR ya
Rwanda bao 2-1.
|
Azam FC : Deo
Munishi ‘Dida’, Ibrahim Shikanda, Erasto Nyoni, Said Mourad, Aggrey Morris,
Jabir Aziz, Tcheche, Salum Abubakar, John Bocco, Ibrahim Mwaipopo, Ramadhan
Chombo
Akiba:
Mwadini Ally, Samir Haji Nuhu, Joseph Owino, Odhiambo, Khamis Mcha, Mrisho
Ngassa, Mwaikimba
|
WAGOMBEA
‘BUTI la DHAHABU.
-Teddy
Etekiama [Vita Club]=Bao 6
-Said
Bahanuzi [Yanga]=6
-Hamisi
Kiiza [Yanga]=6
-John Bocco
[Azam]=5
-Suleiman
Ndikumana [APR]=3
-Preus
[APR]=2
-Abdallah
Juma [Simba]=2
Tangu 2002 rais wa Rwanda, Paul Kagame alipotangaza kudhamini zawadi ya
washindi ya dola 60, 000, ambapo bingwa anapata dola 30,000, wakati mshindi wa
pili Dola 20,000 huku yule wa tatu anapata dola 10,000, mpaka leo zawadi
hizo hazijabadilika.
Source www.mwanawamakonda.blogspot.com
No comments:
Post a Comment