Bw.John Dramani akiapishwa Mahakamani. |
Kiongozi
mpya wa Ghana John Dramani Mahama ameahidi kuimarisha hali ya utulivu kufuatia
kifo cha Rais John Atta Mills. Bw. Mahama mwenye umri wa miaka 53, aliapishwa
saa kadhaa baada ya Rais aliyekuwa na umri wa miaka 68 kufariki hospitalini
mjini Accra.
Upinzani
wa nchini humo umesifu kasi iliyotumiwa katika kufanya mabadiliko
yaliyomkabidhi Bw.Mahama mamlaka ya kuiongoza nchi ya Ghana na kusema kuwa ni
kuonyesha kuwa Ghana ina upevu Kidemokrasi.
Bw.
Atta Mills aliyeiongoza Ghana kuanzia mwaka 2009 alikua na saratani ya koo na
alikua na mipango ya kuwania muhula wa pili katika uchaguzi unaopangwa
kufanyika mwezi disemba.
Mwandishi
wa BBC mjini Accra, Sammy Darko anasema kuwa Rais aliyekabidhiwa wadhifa wa
Rais ataongoza kama Rais hadi wakati wa uchaguzi, ingawa haijafahamika kama
atasimama kama mgombea rasmi wa chama cha NDC(National Democratic Congress.)
Wakati
wa kuapishwa mbele ya kikao maalum cha Bunge kilichoitishwa kwa dharura,
Bw.Mahama aliahidi kuwahudumia raia wote wa Ghana. Punde baada ya kutangazwa
kuwa Rais, Bw.Mahama alitangaza maombolezi ya wiki nzima.
Kiongozi
wa upinzani wa chama cha New Patriotic Party Nana Akufo Addo amesema
ameahirisha kampeni za kugombea kiti cha Rais kwa heshima ya marehemu.
Mwenyekiti
wa NPP Jake Obetsebi-Lamptey amesifu jinsi mabadiliko yalivyofanywa kufuatia
kifo cha Rais.
Ingawa
kulikuepo na mjadala mkubwa kuhusu afya ya Bw.Atta Mills, suala hilo
halikugusiwa rasmi, wanaserma wandishi wa habari. Kiongozi huyo alikanusha
kuhusu maumivu na kusisitiza kua katika hali nzuri ya afya.
Kulingana
na msaidizi wa Rais, marehemu alilalamika kua na maumivu siku ya jumatatu jioni
na tangu hapo hali yake ikazidi kua mbaya.
Source:mwanawamakonda.blogspot.com
No comments:
Post a Comment