Monday, July 30, 2012

Kingwendu


Hebu tukumbuke ya kale


Katibu wa chama cha soka wilaya ya Kakonko(FAKADI) hakiitambui Ligi ya jamii inayochezwa kata ya Kasanda


Katibu  (FAKADI)  Denisa Lazaro.


Na:Issa Ngumba  Kakonko.

Katibu wa chama cha soka wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma  Denisa Lazaro,amesema hatambui ligi ya jamii iliyokuwa ikichezwa katika kata ya Kasanda na kusabisha kifo cha  mchezaji Inocent Daniel aliyekuwa akichezea timu ya Kazilamihunda FC ,aliefia uwanjani wakati timu yake ilipokuwa ikichuana na timu ya Chilambo FC  katika  uwanja wa Kasanda.

 

 

Denisa amesema  kuwa chama cha soka wilaya ya kakonko (FAKADI) hakitahusika na lolote kuhusina na tatizo  hilo lililotokea katika mchezo  huo,kwa  kuwa ligi   hiyo watu wa kasanda walishiriki chini ya uongozi wa soka kutoka  wilaya ya kibondo.

 

 

Aidha  amewataka kusimamisha ligi  hiyo hadi pale watakapopata maelekezo kutoka uongozi wa chama cha soka wilaya ya kakonko (FAKADI) na si kuagizwa na uongozi wa soka wilaya ya kibondo(KDFA).

 

 

Katibu huyo wa FAKADI  Denisa amesema kuwa tayari ofisi yake imepokea fomu za kugombea uongozi katika chama  hicho na amewataka wadau kujitokeza kuchukua fomu  hizo na kwamba  fomu hizo zitalipiwa ada ya shilingi elfu 30 kwa  ngazi ya uongozi na wajumbe shilingi elfu 20.

 

source www.mwanawamakonda.blogspot.com

Gazeti la Mwanahalisi lafungiwa




JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO


TAMKO LA SERIKALI

GAZETI LA MWANAHALISI LAFUNGIWA

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imelifungia kutochapishwa gazeti la MwanaHalisi kuanzia 30 Julai, 2012 kwa muda usiojulikana kutokana na mwenendo wake wa kuandika habari na makala za uchochezi, uhasama na uzushi likiwa na nia ya kusababisha wananchi kukosa imani na vyombo vya dola hali inayoweza kuhatarisha amani na mshikamano uliopo nchini.
Katika matoleo yake hivi karibuni, gazeti la MwanaHalisi toleo Na. 302 la Jumatano Julai, 11 – 18, 2012 na toleo Na. 303 la Jumatano Julai 18 – 24, 2012 na toleo Na. 304 la Jumatano Julai 25 hadi 01 Agosti, 2012 na mengine yaliyotangulia yamekuwa yakichapisha habari na makala zenye kueneza na kujenga hofu kwa jamii.
Mhariri wa gazeti la MwanaHalisi, ameitwa na kuonywa mara nyingi, lakini hataki kukiri kuwa maudhui ya makala zake hazina tija kwa jamii, pia hazifuati weledi na maadili ya taaluma ya uandishi wa habari.
Mhariri, mara zote katika utetezi wake amekuwa akinukuu kifungu cha 18 cha Katiba ya nchi yetu ambacho kinatoa uhuru wa kutoa maoni na kwa makusudi kutonukuu kifungu cha 30 cha Katiba hiyo kinachoweka ukomo wa uhuru.
Uamuzi wa Serikali
Serikali imeamua kulifungia kutochapishwa kwa muda usiojulikana gazeti la MwanaHalisi, kwa mujibu wa Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976, kifungu Na. (25) (i), adhabu hiyo itaanza tarehe 30 Julai, 2012 kwa mujibu wa Tangazo la Serikali (Government Notice) Na. 258 lililochapishwa katika Gazeti la Serikali na kutolewa jijini Dar Es Salaam tarehe 27 Julai, 2012.
Serikali inawataka wamiliki, wahariri na wanahabari kuzingatia sheria, uzalendo, weledi na maadili ya taaluma ya uandishi wa habari katika kutekeleza wajibu wa kuhabarisha, kuelimisha na kutoa burudani kwa wananchi.
Kama ilivyoelezwa Bungeni wakati wa kuwasilisha Bajeti ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo hivi karibuni waandishi na watangazaji wa habari wanatakiwa kuhakikisha kuwa habari wanazoziandika na vipindi wanavyoandaa vinazingatia taaluma na kuweka mbele maslahi ya Taifa letu na uzalendo. Uhuru na haki ya vyombo vya habari uendane na wajibu.
Kuanzia sasa Serikali haitasita kuchukua hatua dhidi ya vyombo vya habari ambavyo kwa maksudi vitatoa taarifa za uchochezi ambazo zitahatarisha hali ya amani na utulivu uliopo nchini mwetu.

Imetolewa na

OFISI YA MSAJILI WA MAGAZETI
WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO

Sunday, July 29, 2012

Tazama Yanga katika picha waki shangilia ubingwa wa Kombe la Kagame 2012

Kikosi cha Yanga kilicho tetea ubingwa wa kagame

Saidi Bahanuzi mfungaji bora wa mashindano ya kombe la Kagame 2012

Wachezaji wa Yanga wakishangilia goli na mashabiki wao

Ubao wa matangazo wa uwanja wa Taifa ukionyesha matokeo ya mchezo

Ally Mustapha akiudaka mpira

Kocha wa Yanga TOM Santfiet kulia na kocha wa Azam Sittwart Hall kushoto wakizungumza baada ya mechi

Wachezaji wa Yanga wakishangilia ubingwa wa Kagame 2012

Wachezaji wa Yanga wakishangilia Ubingwa wao baada ya kuilaza Azam magoli 2-0

Wachezaji wa Yanga wakiwaonyesha mashabiki ubingwa wa kagame

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Said Meki Sadik akimkabidhi nahodha wa Yanga Nadir Haroub ubingwa wa Kombe la Kagame

Agrey Moris wa Azam na Hamis Kiiza wa Yanga wakigombania mpira

wachezaji wakikimbiza kombe la kagame
Picha kwa hisani ya mitandao mbalimbali

Saturday, July 28, 2012

Yanga ni Bingwa tena Kagame Cup yaipiga Azam 2-0


Yanga: Ally Mustapha 'Barthez', Stephano Mwasika, Oscar Joshua, Nadir Haroub 'Cannavaro' (C), Kelvin Yondan, Athuman Idd 'Chuji', Rashid Gumbo, Haruna Niyonzima, Said Bahanunzi, Hamis Kiiza 'Diego', David Luhende - 29.

Akiba: Yaw Berko, Ladislaus Mbogo, Juma Seif 'Kijiko', Idrisa Rashid, Shamte Ally, Nizar Khalfan, Jeryson Tegete



Klabu ya Soka ya Yanga  leo kwenye Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam wamefanikiwa kutetea vizuri  Taji lao la Klabu Bingwa Afrika ya Mashariki na ya Kati walipoitandika Timu ngumu ya Azam FC bao 2-0 kwenye Fainali na kuendelea kubaki na kombe hilo la KAGAME  baada ya kulitwaa Mwaka jana walipowafunga Mahasimu wao  wakubwa Simba kwa  bao 1-0.

Aidha Wafungaji  wa Yanga leo ni Mastraika wao hatari sana, Hamisi Kiiza na Said Bahanuzi, ambao ndio walipachika bao za leo na kila mmoja kufikisha Bao 6 wakifungana na Teddy Etekiama wa Vita Club ya DRC kwa kuwa ndio Wafungaji Bora wa Mashindano haya.

Bao la kwanza la Yanga lilifungwa na Hamisi Kiiza katika Dakika ya 44 na Said Bahanuzi akapiga Bao la pili katika Dakika ya 90.

Mwenyekiti mpya wa Yanga, Yusuf Manji.

 

Hakika hii ni chereko kubwa huko Jangwani kwa Mwenyekiti mpya wa Yanga, Yusuf Manji, na Kocha wao mpya Tom Saintfient kwani huu ulikuwa ni mtihani wao mkubwa wa kwanza tangu watwae nyadhifa zao hivi karibuni.


Kikosi cha Vita Club ya Congo DR.

 

Katika Mechi ya awali ya kusaka Mshindi wa Tatu, Vita Club ya Congo DR iliifunga APR ya Rwanda bao 2-1.

Azam FC : Deo Munishi ‘Dida’, Ibrahim Shikanda, Erasto Nyoni, Said Mourad, Aggrey Morris, Jabir Aziz, Tcheche, Salum Abubakar, John Bocco, Ibrahim Mwaipopo, Ramadhan Chombo

Akiba: Mwadini Ally, Samir Haji Nuhu, Joseph Owino, Odhiambo, Khamis Mcha, Mrisho Ngassa, Mwaikimba

 

WAGOMBEA ‘BUTI la DHAHABU.

-Teddy Etekiama [Vita Club]=Bao 6

-Said Bahanuzi [Yanga]=6

-Hamisi Kiiza [Yanga]=6

-John Bocco [Azam]=5

-Suleiman Ndikumana [APR]=3

-Preus [APR]=2

-Abdallah Juma [Simba]=2

 

Tangu 2002 rais wa Rwanda, Paul Kagame alipotangaza kudhamini zawadi ya washindi ya dola 60, 000, ambapo bingwa anapata dola 30,000, wakati mshindi wa pili  Dola 20,000 huku yule wa tatu anapata dola 10,000, mpaka leo zawadi hizo hazijabadilika.

Source www.mwanawamakonda.blogspot.com

Tazama habari mbalimbali katika picha nzuri na za kuvutia


Hawa ni Ngombe wakipatikana Tanzania ,licha ya nyama yao kuwa tamu ila supa star kawa kuku’


Kucheza na  mwinzio huwa raha sana hasa pale mnapokuwa mmepumzika kwa wanyama huwa ni jambo la furaha sana.

 


Anajulikana kama Tiger mnyama jamii ya chui lakini mabaka yake ni tofauti.

 


Moja ya vivutio vinavyoifanya Tanzania kuwa nchi ya kipekee duniani ni msimu wa kuhama wanyama jamii ya nyumbu toka mbuga za ngorongoro na serengeti ambao kila mwaka huvuka mto Mara kuingia nchini Kenya kwa ajili ya kupisha kiangazi. Hili ni moja ya tukio ambalo limeingizwa katika maajabu 10 ya asili duniani. Pichani ni baadhi ya nyumbu wakianza kuvuka.



Mwanza: moja ya majiji masafi kabisa Tanzania huku kukiwa na adhabu kubwa kwa wote wanaoshindwa kuweka mazingira yao katika hali usafi. Ni kwa nini Mwanza au Moshi wameweza lakini majiji mengine kama Dar es Salaam bado yanaendelea kutokuwa na mazingira safi?


Watanzania na Waafrika wengi kwa ujumla asili ya malezi ya mtoto ilikuwa inahusisha mtoto wa kunyonyeshwa na mama na pia kubebwa mgongoni hadi atakapofikia umri wa kuweza kutembea mwenyewe.


Hapooo  sasa patamu mdau’’97.9FM Ngara,Rwanda’’93.6 FM Kibondo na Burundi,94.2 FM Kasulu,Kigoma ujiji,Mashariki mwa DRC >>Sikilizeni RK live kwenye www.radiostationstz.com’ ‘’upate radha na utamu wa burudani,elimu na taarifa mbalimbali za kijamii,huku tukipanda mbegu za matumaini na JUKWAA LA MATUMAINI’


Picha imepigwa nikiwa nimesimama "mtaa" uitwao NYAMIAGA wilayani Ngara mkoani Kagera, maana ipo juu kidogo na ni karibu na NYAMIAGA shule ya msingi'' kama sikosei.... …..HAPA NI HADITHI YA MVUVI NA SAMAKI WA DHAHABU bana !!!


Duh! kaazi kwelikweli najiuliza mpaka sasa kesho kutwa ni miaka 50 ya UHURU lakini...MWANAMKE KWELI NI MWANAMKE..

Picha inamuonesha mama akikabiliwa na majukumu mazito kama anavyoonekana katika picha hii.Ingawa mama huyu anakabiliwa na changamoto mbalimbali bado anaonekana mwenye furaha.


Karibu Tanzania ,Katavi Hippo  .



Tupende wanyama wa nchi yetu kwa pamoja inawezekana .

Hivi ni Vichali vya ndege watuamshao asubuhi kwa milio ya aina tofauti kuashiria kumepambazuka.

source mwanawamakonda.blogspot.com