NgaraSerikali
wilayani ngara imeanza zoezi la kuwakamata wazazi ambao hawajawpeleka
shule wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na masomo ya sekondari kwa
ajili ya chukuliwa hatua za kisheria.
Akizungumza na mwandishi wa
habari hii ofisini kwake kaimu katibu tawala wa wilaya ya Ngara david
mafipa amesema zoezi hilo litaanza katika kata za murukulazo,ntobeye na
kumalizia kata ya kanazi.
Bw.Mafipa amesema kuwa asilimia 40 ya
wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu
hawajaripoti katika shule walizopangiwa.
Alinukuliwa akisema
"TUTAWAKAMATA KAMA TULIVYO AHIDI NA TUWAPELEKA KATIKA VYOMBO VYA SHERIA WAKAJIBU MASHTAKA,KAMA TULIVYOSEMA KWAMBA TUTAAKIKISHA HAKI ZA WATOTO WANAPATA IKIWEMO HAKI YA ELIMU NI WAJIBU WA MZAZI KUAKIKISHA MWANAE ANAKWENDA SHULE"
"TUTAWAKAMATA KAMA TULIVYO AHIDI NA TUWAPELEKA KATIKA VYOMBO VYA SHERIA WAKAJIBU MASHTAKA,KAMA TULIVYOSEMA KWAMBA TUTAAKIKISHA HAKI ZA WATOTO WANAPATA IKIWEMO HAKI YA ELIMU NI WAJIBU WA MZAZI KUAKIKISHA MWANAE ANAKWENDA SHULE"
Aidha amesema zoezi hilo ni endelevu na litafanyika kwa
wilaya nzima ili kuwabaini wazazi ambao wameshindwa kuwapeleka watoto
wao shule kutokana na visingizio mbalimbali ili wafikishwe katika vyombo
vya sheria
Kwa upande wao wananchi walikipongeza kitendo cha
serikali wilayani ngara kuwachukulia hatua wazazi ambao hawajawpeleka
shule watoto wao waliochaguliwa kujiunga na masomo ya sekondari
nakuiomba serikali ijizatiti kwa zoezi hilo kutokana na zoezi hilo kuwa
gumu.
Mmoja ya wananchi Bw.Goerge Andrew alisema kuwa serikali inatakiwa kujizatiti vilivyo kwa ajili ya zoezi hilo
"Kiukweli
serikali yetu imefanya jambo zuri kutokana na umuhimu wa elimu kwa
watoto kwa sasa ila inatakiwa ijizatiti kutokana na wazazi wengine
wasioelewa kuwaficha watoto ama kukimbia"
No comments:
Post a Comment