NGARA
Wakazi wa kijiji cha Murubanga kata ya Murusagamba wilayani
Ngara huenda wakakumbwa na baa la njaa kutokana na kundi la tembo kushambulia
zaidi ya ekari 60 za mahindi kijijini humo
Diwani wa kata ya Murusagamba Bw Soud Mkubila amesema kuwa
tembo wanaokadiriwa kufikia 50 wamevamia eneo la Mulonzi yaliko mashamba mengi
ya wakazi wa kijiji cha Murubanga
Amesema taarifa kuhusu uharibifu huo zimetolewa kwa
halmashauri ya wilaya ya Ngara ili wataalamu wende kuwafukuza tembo hao
waliovamia kijijini humo tangu juzi na kusababisha hofu kwa wanakijiji
Bw Mkubila amesema kuwa wataalam wa idara ya wanyamapori
kutoka halmashauri ya wilaya ya Ngara wamekwenda kijijini humo leo kwa ajili ya
kuwafukuza tembo hao na kufanya tathmini ya uharibifu uliojitokeza
No comments:
Post a Comment