Mrisho Salum
Ngara-kagera
Katibu wa chama cha wapanda pikipiki wilayani Ngara Bw
Castory Paschal amewataka wapanda pikipiki wilayani humo kujenga kawaida ya
kutii sheria bila shuruti ili kuepuka mikwaruzano na vyombo vya sheria na
kuepuka ajali zinazoweza kuepukika
Akizungumza na mjukuu wa tozo Bw Paschal amesema kuwa wapanda pikipiki wengi
wilayani humo hawana elimu ya kutosha kuhusu usalama barabarani hali
inayosababisha kuendelea kutokea kwa ajali zisizokuwa za lazima.
Alisema kuwa baadhi ya wapanda pikipiki wamekuwa wakikiuka
taratibu kwa kutovaa kofia ngumu, kupakia abiria zaidi ya mmoja pamoja na
kutokuwa na kofia ya abiria wake
Alinukuliwa akisema
“KUNA BAADHI WANAUTUHARIBIA
UTARATIBU TULIOJIWEKEA WANAPAKIA ABIRIA ZAIDI YA MMOJA HASA NYAKATI ZA USIKU
HALI INAYOWEZA KUSABABISHA AJALI.”
Aidha amewashauri wapanda pikipiki kutovunja sheria za
usalama barabarani kwani kufanya hivyo kunapelekea ajali zisizikuwa za lazima
na kupoteza nguvu kazi ya taifa.
Pamoja na mambo mengine Bw Pashal alisema kuwa wapanda pikipiki hao wanatarajiwa kufanya
uchaguzi ili kupata viongozi wapya katika mkutano utakaofanyika katika ukumbi
wa Community Centre mjini Ngara
No comments:
Post a Comment