Sunday, February 24, 2013

WALIMU WATAKIWA KUTAMBUA WAJIBU WAO



Na James jovin
KIBONDO
Paroko Christopher Ndizeye wa parokia ya Kibondo mkoani Kigoma amewataka walimu kutambua kuwa ualimu ni wito hivyo wanatakiwa kuifanya kazi hiyo kwa moyo na uzalendo ili kuinua kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi

Padre Ndizeye amesema hayo juzi  alipokuwa mgeni rasmi katika mahafali ya tisa ya kidato cha sita katika shule ya sekondari ya wasichana Bon Konsil wilayani Kibondo

Amesema iwapo walimu watafanya kazi zao kwa moyo wa dhati na kuweka uzalendo mbele watasaidia wanafunzi kupenda masomo hali itakayoinua kiwango cha taaluma nchini


Kwa upande wake mkuu wa shule hiyo Sister Generoza Mpilirwe ametoa wito kwa serikali kutafuta kiini cha kushuka kwa kiwango cha ufaulu kila mwaka na kutafuta ufumbuzi wa tatizo hilo

No comments:

Post a Comment